Monday, July 6, 2015

MWENGE WAZINDUA MIRADI YA THAMANI YASHILINGI BILIONI KUMI NA TATU NJOMBE



Miradi ya Shilingi billion Kumi na  tatu (13,201,109,235.55) inatalajiwa kuzinduliwa,kuwekewa jiwe la Msingi na kukaguliwa na mbio za Mwenge wa Uhuru katika Mkoa wa Njombe,hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Njombe  Dk.Rehema Nchimbi wakati akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka Mkoa wa Iringa.
Nchimbi alisema kuwa Mwenge wa Uhuru katika Mkoa wa Njombe utakimbizwa katika halmashauri Sita ambazo ni Njombe,Makete,Ludewa,Wanging’ombe,Mji Njombe  na Mji Makambako,Katika halmashuri jumla ya
Miradi 45 itatembelewa na Mwenge wa Uhuru.
Alisema kuwa Miradi hiyo ipo katika sekta ya Afya ,Elimu,Kilimo,Miundombinu,Utalii na Misitu,miradi mingi imekamilika na kuanza kutumika .
Naye mkimbiza Mwenge Kitaifa  Juma Khatibu chum alisema kuwa amefurai kuingia Mkoa wa Njombe  na anarajia kufungua,kukagua miradi mizuri kwani kutokana na mapokezi walioyapata ya wananchi wengi  waliojitokeza kuupokea Mwenge wa Uhuru, Kauli mbiu ya Mwenge Mwaka huu ni “Tumia haki yako kidemokrasia ,Jiandikishe  na kupiiga kura katika uchaguzi wa mwaka 2015.




No comments:

Post a Comment

Popular Posts