Thursday, March 12, 2015

BASI LA MAJINJA EXPRESS LAPATA AJALI MUFINDI



001
Umati wa watu wakisubiri kutambua maiti za watu waliofariki katika ajali ya basi la Majinja Express katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya wilaya Mufindi.




002

 Baadhi ya ndugu waliopoteza ndugu zao katika ajali ya basi la Majinja Express wakilia kwa uchungu mara baada ya kujua kuwa moja wa ndugu zao wamefariki dunia.

 003
 Mmoja wa majeruhi ambaye jina lake halijatambulika akiwa katika hospitali ya wilaya Mufindi kwa matibabu zaidi.



004

 Mmoja wa majeruhi ambaye hali yake mbaya akipakizwa katika gari la wagonjwa kupelekwa kwa matibabu zaidi hospitali ya rufaa ya mkoa wa Iringa kwa matibabu zaidi.


 005

Umati wa watu wakiwa katika eneo la tukio mara baada ya ajali kutokea eneo tukio ambapo ajali ya basi la Majinja limepoteza watu 42 katika ajali hiyo.
(Picha na Denis Mlowe)



 
 
 
 










Mpaka saa hizi naambiwa na watu wa Iringa idadi ya waliokufa katika ajali hiyo ni 42 na maiti 32 ambazo hazijitambuliwa zimefikishwa hospitali ya mkoa wa Iringa kutoka Mafinga.
Moja wa mashuhuda wa ajali hiyo Jackson Manga alisema kama dereva wa basi hilo angezingatia ishara za taa kali alizokuwa akiwashiwa na dereva wa roli hilo kwa vyovyote vile ajali hiyo isingetokea.
Manga alisema katika eneo hilo lenye mteremko wa wastani, roli lilikuwa likipandisha na basi lilikuwa likishuka.
 
 
Alisema ukaidi wa dereva wa basi ulisababisha dereva wa roli aingie katika shimo kubwa katika eneo hilo hali iliyosababisha ashindwe kulimudu gari hilo kabla ya kuvaana uso kwa uso na basi hilo.
“Baada ya kuvaana, kontena la futi 40 lililokuwa limepakiwa katika roli hilo liliruka juu na kwa kishindo kikubwa, kubamiza na kufunika basi hilo,” alisema.
Mmoja wa majeruhi wa basi hilo, Kevin Humphrey ambaye kalazwa katika hospitali ya wilaya ya Mufindi alisema; “tulisikia mshindo mkubwa baada ya basi letukugongana na roli hilo na mshindo huo ulisababisha na kontena iliyotoka kwenye roli hilo na kupiga juu ya basi letu.”















 

No comments:

Post a Comment

Popular Posts