Tuesday, June 16, 2015

AJALI YA ANOTHER G MAFINGA ,WATU 25 WAFARIKI


 Image result for ajali ya another G mafinga

UZEMBE wa dereva wa basi Mitsubishi Fuso, mali ya kampuni ya Another G Trans lenye usajili Namba T.927 CEF, Nicolaus Magula (30) umesababisha abiria 23 wapoteze maisha na wengine 34 kujeruhiwa vibaya katika ajali iliyotokea juzi Jumapili mjini Mafinga.
Ajali hiyo ilitokea Majira ya saa 1.45 usiku katika eneo la Kinyanambo A, barabara Kuu ya Iringa Mbeya baada ya basi hilo kugongana uso kwa uso na  na roli aina ya Scania lenye namba za usajili T.916 AQM likiwa na tela namba T 965 BEH, mali ya kampuni ya Bravo Logistics (T) Ltd ya Dar es Salaam.
Wakati ajali hiyo ikitokea, wakazi wa Mafinga na Tanzania kwa ujumla bado wanakumbuka ajali nyingine iliyotokea katika eneo la Changarawe, mjini Mafinga miezi mitatu iliyopita (Machi 11, mwaka huu) ikuhusisha roli Scania namba T 689 APJ mali ya Cipex Company na basi Scania namba T 438 CED  na kusababisha vifo vya watu 50.
Akizungumza na wanahabari jana, Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa Pudenciana Protas alisema; “wakati basi hilo lenye uwezo wa kupakia abiraia 65 lilikuwa likitokea Iriinga kuelekea Njombe, roli hilo lililokuwa likiendeshwa na Rogers Wales mwenye miaka 39, Msambaa mkazi wa Mwanza lilikuwa likitokea barabara kuu ya Mafinga kuelekea Iringa.”
Protas alisema chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva wa basi hilo aliyekosa umakini na kutaka kulipita gari lingine bila kuchukua tahadhari.
Alisema miili ya marehemu na majeruhi hao ilikimbizwa katika hospitali ya wilaya ya Mufindi ya mjini Mafinga, mapema baada ya ajali hiyo kutokea.
Alisema miili 12 ya watu waliokufa imekwishatambuliwa na kuwataja kuwa ni pamoja na Lucas Pancras, Blasto Samila, Dickson Luvanda, Albert Silla (askari wa Ruvu JKT), Eva Mbalinga, Khadija Mkoi (4), Clemence Mtati, Mohamed Lalika, Castory Mwakiamba, Damiana Myala na Silo Nziku ambao wote walikuwa katika basi hilo na dereva wa roli hilo Rogers Wales.
Alitaja majeruhi wa ajali hiyo waliokuwa katika basi hilo kuwa ni pamoja na Emma Lupembe (35), Veronica Simba (20), Shafia Ally (24), Mariamu Mbise (23), Anita Makwela (24), Benita Sagara (18), Bertha Mkoi (27), Rahel Mavika (18),, Selina Fulgensi (23), Maria Mwenda (17), Ndipako Mbilinyi (28), Alexander Mkakazi (28), Meshack Kibiki (44), Simoni Jumbe (22), Jerry Lutego (36), Enock Kanyika (18) na Yusuph Lulandala (22).
Wengine ni Deogratias Kayombo (21), Petro Mwalongo (21), Paul Chahe (21), Kennedy Msemwa (28), Emanuel Anthony (21), Mode Shilazi (21), Godfrey Kanyika (39), Boniface Bosha (20), Ambiana Meshack (35), Martha Kanyika (30), Melika Tonga (2.5), Yusuph Luhumba (34) na Damiana Kuyala (42).
Protas alisema majeruhi wengine wanne, wanaume wawili na wanawake hawajatambuliwa majina yao kwasababu walikuwa hawaongei
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

No comments:

Post a Comment

Popular Posts