Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dk.Rehema
Nchimbi amewataka watumishi
walioamishiwa na walioajiliwa katika
halmashuri ya Wiaya ya Wanging’ombe kuakikisha wamehamia kimakazi katika wilaya hiyo.
Dk.Rehema Nchimbi,amesema
kuwa wananchi wa Wilaya ya Wanging’ombe
watakiwa kupata huduma kutoka kwa watumishi hao na anashangaa kuona
watumishi wanaishi Njombe mjini na kufanyakazi katika halmashuri ya wilaya ya
Wanging’ombe ambayo ipo zaidi ya umbali wa kilometa 40 kutoka Njombe Mjini.
Nchimbi ametoa wiki
mmoja toka leo kuakikisha watumishi hao wawe wameamia na kuishi katika Wilaya
hiyo ili kuongeza ufanisi wa kazi na kuwa karibu na wananchi ,aliyasema hayo
kwenye ukumbi wa halmashuri ya wilaya ya Wang’ingombe wakati akifanya mkutano
wa watumishi wa halmshauri hiyo.
Naye Mkuu wa Wilaya ya
Wanging’ombe Fedrick Mwakalebela alisema
kuwa wilaya hiyo inamahitaji yote muhimu
kama vile ofisi,miundombinu ya maji na barabara na kuwasihii watumishi hao wakikishe wanahami
katika wilaya hiyo haraka iwezekanazo kwani maendeleo ya wanging’ombe yataletwa
na wananchi wa wanging’ombe kwa kushilikiana na watumishi.
Mkurungenzi wa Wilaya
hiyo Melizedeki Humbe alisema kuwa
watumishi wengi katika wilaya hiyo bado wanaishi Njombe mjini lakini wamewaka
mikakati ambayo ndani ya wiki mmoja waliopewa kuakikisha watumishi hao wote
wanaamia katika wilaya hiyo mpya iliyo anzishwa mwaka 2012.
No comments:
Post a Comment