Wednesday, June 17, 2015

PINDA APATA WADHAMINI NJOMBE




Mgombea wa Urais kupitia chama cha mapinduzi na waziri Mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda amewataka wananchama wa chama  cha mapinduzi Mkoa wa Njombe kuendelea kujitokeza kwa wingi na kuendelea kuwadhamini wagombea mbalimbali  waliochukua fomu na watakaochukua fomu  za kugombea nafasi ya  Urais bila kubagua Mgombea yoyote.
Waziri Mkuu ameyasema hayo leo kwenye ukumbi wa chama cha mapinduzi Mkoa wa Njombe ambapo mamia ya wananchama wa chama hicho  walijitokeza kumdhamini ili aweze kugombea Urais kupitia chama cha Mapinduzi
Alisema kuwa waliojitokeza kuchukua fomu kupitia chama cha mapinduzi ni wengi lakini atakayepitishwa kupitia chama hicho ni mgombea mmoja ambaye atawakilisha chama cha Mapinduzi kwenye uchaguzi unatakofanyika mwezi wa kumi na mgombea huyo ndie atanadiwa na chama hicho akishindanishwa na vyama vingine  kwenye uchaguzi Mkuu.
Wanachama waliojitokeza kumdhamini Mgombea huyo wamesema kuwa wanaimani kubwa na mgombea huyo na kuamini kuwa chama kitampitisha kuwakilisha chama hicho kwenye kugombea Urais.
Kwa Mkoa wa Njombe tayari wagombea January Makamba,Bernard Membe,Stive Wassira,Samweli Sitta,Makongoro Nyerere ,Monica Mbega ,Amosi Siyatemi na Prof.Mark Mwandosya.










No comments:

Post a Comment

Popular Posts