Tuesday, June 23, 2015

Ngassa arejea Yanga kiaina








Mshambuliaji wa Free Stars ya Afrika Kusini,Mrisho Ngassa (kulia) akifanya mazoezi na timu yake ya zamani Yanga baada ya kurejea nyumbani kwa mapumziko kwenye uwanja wa karume Dar es Salaam Jana.Picha na Said Khamis. 



Dar er Salaam. Mshambuliaji Mrisho Ngassa aliyesajiliwa na klabu ya Free State Stars ya Afrika Kusini hivi karibuni, jana aliibuka katika mazoezi ya timu yake ya zamani Yanga.
Ngassa alisajiliwa na Free State Stars kwa mkataba wa miaka minne mwishoni mwa mwezi uliopita na alirudi nchini kwa ajili ya kuitumikia Taifa Starsiliyokuwa ikicheza dhidi ya Uganda katika mechi ya kuwania kufuzu kushiriki fainali za Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani (CHAN), ingawa Shirikisho la Soka Afrika (CAF) lilimzuia kwani ameishasajiliwa nje ya ligi ya Tanzania.
Gazeti hili lilimshuhudia mshambuliaji huyo akifanya mazoezi na Yanga mwanzo mwisho na alipomaliza mashabiki wa klabu hiyo walilisukuma gari lake mpaka nje geti wakionyesha mapenzi kwa mchezaji huyo.
Ngassa ameitumikia Yanga kwa mafanikio kabla ya kuamua kuachana nayo na kwenda kusaka ulaji katika klabu ya Free State.
Ngassa alisema ameamua kufanya mazoezi na Yanga kwani bado iko moyoni mwake na hakuondoka kwa ubaya.
“Hapa kama niko nyumbani, kwani hii ni timu iliyo moyoni mwangu hivyo kama niko Dar es Salaam sioni ubaya kufanya mazoezi na Yanga kwani naamini kuna siku nitarudi hapa,”alisema Ngassa.
“Najiweka fiti wakati nikisubiri klabu yangu initumie tiketi ya kurudi Afrika Kusini maana walinipa ruhusa ya kuja Dar es Salaam kwa ajili ya timu ya Taifa, lakini nikazuiwa kucheza mechi na Uganda,” alisema Ngassa.
Msimu uliopita haukuwa mzuri kwa Ngassa kwani aliifungia Yanga mabao manne tu licha ya kuchaguliwa kuwa mchezaji bora wa Aprili

















No comments:

Post a Comment

Popular Posts