Saturday, July 26, 2014

BREAKING NEWS : BASI LA HOOD LAPATA AJALI MBAYA ASUBUHI HII LIKITOKEA MBEYA


 Muda mchache baada ajali kutokea 












  Askari wa usalama wa barabarani wakiwa wamefika eneo la tukio  na baadhi ya Mashuhuda wakishuhudia ajali hiyo







 


 Basi la Hood limepata ajali asubuhi hii likitoka Mbeya haijafahamika mara moja lilikuwa linaelekea wapi na haijafahamika kama kuna watu waliojeruhiwa, endelea kufutilia hapa kupata taarifa kamili hii ni taarifa ya awali.

Picha na Mbeya yetu Blog














Friday, July 25, 2014

Maandamano makubwa yamefanyika katika ukingo wa Magharibi mwa Palestina karibu na mpaka wake na Israel kupinga mashambulio yanayofanywa na Israel.

Waandamanaji hao wakiwa na hasira wakiwa Gaza walipambana na vikosi vya usalama vya Israel.
Hata hivyo mapambano makubwa dhidi ya vikosi vya usalama ilikuwa katika eneo la Qalandia katika mpaka wa Ramallah and Jerusalem.
Raia mmoja wa Palestinian ameuawa katika maandamano hayo huku wengine kadhaa wakijeruhiwa .
Takriban wapaelestina 800 wameuawa tangu kuanza kwa mashambulizi ya Israel huko Gaza mapema mwezi huu.

Mabaki ya ndege iliyopotea ikiwa na watu 116 njiani kutoka Burkanafaso kwenda Algers yamepatikana nchini Mali.

Maafisa wa Jeshi wa Burkina faso wamesema ndege hiyo iliyokuwa chini ya shirika la ndege la Algeria imeanguka karibia kilomita 50 kutoka mpaka wa Burkanafaso.
Waongoza ndege walipoteza mawasilino na ndege hiyo muda mfupi baada ya kupata taarifa kutoka kwa Rubani kuwa alikuwa kwenye eneo lenye hali mbaya ya hewa.
Utafutaji wa ndege hiyo umeanzia katika eneo la Gao mpaka Tessalit. Kumekuwepo na hali mbaya ya hewa kwa zaidi ya saa 24. Waziri wa mambo ya nje wa ufaransa, Laurent Fabius amesema inaonekana ndege ilihamishwa mwelekeo kwa sababu ya hali mbaya ya hewa.
„Walikuwa wameelekezwa kubadili njia ya kawaida kutoka na mabadiliko ya hali ya hewa.Ndege ilikuwa ikipaa juu ya eneo la Malian. Pamoja na juhudi kubwa , mapaka sasa hakuna dalili za kupatika na kwa ndege hiyo. Pengine ndege imeangua"
Ameongeza kuwa waziri wa ulinzi wa ufaransa alikuwa akisaidia katika utafutaji wa ndege hiyo.
"Waziri wa ulinzi wameviruhusu vyombo vyao kwenda kwenye eneo kuitafuta ndege. Majeshi ya Algeria na Umoja wa mataifa wanafanya hivyo pia. Ndege mbili za jeshi la ufaransa zilizopiga kambi Niyame hivi sasa na tangu asubuhi zimekua zikiitafuta ndege hiyo. Majeshi yetu katika eneo hilo ikiwamo vifaa vya matibabu vyote viko tayari"
Hapo awali, waziri mkuu wa Algeria Abdelmalek Sellal alitoa ufafanuzi wa tukio la kuanguka kwa ndege hiyo.
"Usiku wa jana kama saa 9 ndege ya Hispania iliyokodiwa na Shirika la Ndege la Algeria ilikuwa katika safari yake kati ya Ouagadougou na Algiers. Ilipoteza mawasiliano na Rada muda huo wa saa tisa usiku dakika 10 tu baada ya kupaa. Mawasiliano ya mwisho ilikuwa na mnara wa kuongozea ndege ulioko Niger na ndege ilikuwa juu ya Gao, kama kilomita 500 kutoka kwenye mpaka wa Algeria. Kulikuwa na abiria 119 wakiwamo wafanyakazi wake. Utafutaji bado unaendelea na tunawasiliana na mamlaka zinazohusika. Waliokuwa kwenye ndege ni raia wa Algeria pamoja na mataifa mengine"
Mamlaka zinazohusika nchini Burkina Faso ambako ndiko ndege ilitokea wameamua kutoa msaada wa kisaikolojia kwa wanafamilia wa wale waliokuwa katika ndege. Baadhi ya ndugu wamefika katika uwanja wa ndege wa Ouagadougou kufuatilia taarifa kuhusu ndugu zao. Baadhi walikuwa na malalamiko
"Tuwanataka watuambie kama ndege hiyo imeanguka, kuna walionusurika, au wote wamekufa. Hayo ndio tunayotaka kujua. Tupo kwenye wakati mgumu. Watatu miongoni mwetu, tulitaka kusafiri na dada yetu lakini tuliamua kuahirisha safari katika dakika za mwisho. Hata hivyo dada yetu yeye aliondoka usiku jana."
Mwaume mwingine aliyekuwepo kwenye uwanjahuo wa ndege alisem
a

MBUNGE MGIMWA ATUMILIA MILIONI 42 KWA MIEZI MIWILI KUTEKELEZA AHADI



 Katibu  wa  mbunge wa  jimbo la Kalenga Bw Martine Simangwa  kushoto akikabidhi sehemu  bati kwa  viongozi wa kijiji  cha Makota kata ya Mseke

 

 katibu  wa  mbunge Mgimwa Bw  Simangwa akizungumza na  wananchi wa kijiji cha Malagosi 

 

 Sehemu ya saruji  iliyotolewa na  mbunge Mgimwa


 
 Mbunge Mgimwa wa pili  kulia   kulia akikabidhi msaada wa  Saruji kwa  viongozi wa kata ya Nzihi  

 
 Mbunge Mgimwa akiwa katika  usafiri wa Baiskeli 

MBUGE wa  jimbo la kalenga  Gopdfrey Mgimwa ametumia  zaidi ya  Tsh milioni 42   kutekeleza ahadi mbali mbali zilizoachwa na  marehemu babake Dr Wiliam Mgimwa.

Mbunge  Mgimwa amefananikiwa  kutekeleza ahadi hizo ndani ya kipindi  kifupi  cha miezi miwili  toka alipoapishwa  kuwa  mbunge wa  jimbo hilo









 

HAKUNA VITA KATI YA TANZANIA NA MALAWI

RAIS Jakaya Kikwete amesema kamwe Tanzania haitatumia nguvu kumaliza mvutano kati yake na Malawi kuhusu mpaka kati ya nchi hizo, huku akiongeza kuwa, Tanzania haioni mantiki ama busara yoyote kuingia vitani na nchi yoyote jirani kwa sababu yoyote ile.
Alitoa uhakikisho huo kwa Malawi na nchi nyingine jirani wakati alipohutubia mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na mamia kwa mamia ya wananchi kwenye Uwanja wa Michezo wa mjini Mbamba Bay, Mji mkuu wa Wilaya mpya ya Nyasa, juzi. Mji huo uko kwenye pwani ya Ziwa Nyasa.
Rais Kikwete ambaye alikuwa anasemea juhudi za kutafuta ufumbuzi wa suala la mpaka kati ya Tanzania na Malawi, alisema: “Nataka kuwatoeni wasiwasi. Hakuna sababu ya vita.Laleni usingizi bila wasiwasi, kuleni samaki wenu kwa sababu Tanzania haioni busara ya vita.”
“Tanzania haiwezi kutumia nguvu kupata suluhisho la mvutano wa mpaka. Tuna uwezo wa kupata jawabu la tatizo hilo bila kutumia njia ya vita. Tanzania haioni busara hiyo ya vita. Tuna uwezo wa kupata ufumbuzi kwa njia ya majadiliano. Na wala msimamo huo siyo kwa mpaka wetu na Malawi pekee bali kwa mipaka yote ya Tanzania,” alisema Rais Kikwete.
Rais Kikwete pia ameelezea juhudi ambazo zimekuwa zinafanywa na Tanzania kutatua tatizo hilo la mpaka ikiwa ni pamoja na kuliomba jopo la Marais wastaafu kusaidia kutafuta jawabu la mpaka kati ya nchi hizo mbili.
Marais hao Joachim Chissano wa Msumbiji, Festus Mogae wa Botswana na Thabo Mbeki wa Afrika Kusini wanasaidiwa na jopo la Kimataifa la mabingwa wa Sheria katika kazi yao hiyo.
Rais pia amewahakikishia wananchi wa Wilaya ya Nyasa kuwa ahadi na mpango wa Serikali kununua na kuweka meli mpya katika Ziwa Nyasa uko pale pale na kwamba mipango inafanywa ya kuhamisha chelezo cha kujengea meli kutoka Mwanza kwenye Ziwa Victoria kuipeleka Itungi, Kyela, Mbeya ili kuanza ujenzi wa meli hiyo.



















 

Rais ambaye katika Kampeni ya Uchaguzi Mkuu Mwaka 2010 aliahidi ununuzi wa meli tatu za kutoa huduma katika maziwa makuu ya Tanzania ya Victoria, Tanganyika na Nyasa amesema kuwa kiasi cha Sh bilioni 23 zimetengwa tayari kwa ajili ya kuanza ujenzi wa meli hiyo.
Amesema kuwa michoro ya meli hiyo ya Ziwa Nyasa imelazimika kubadilishwa kidogo kwa sababu ya ukweli kuwa ziwa hilo lina mawimbi makali na huchafuka mara kwa mara tofauti na maziwa Victoria na Tanganyika.
Rais Kikwete pia amewaambia wananchi kuwa Serikali inaendelea na mipango ya kujenga reli kutoka Mtwara hadi Mbamba Bay ili kuzidi kufungua ukanda wa Mtwara na kuweza kubeba chuma na makaa ya mawe kutoka Liganga na Mchuchuma, maeneo yaliyoko katika Mkoa wa jirani wa Njombe na wilaya jirani za Nyasa na Ludewa katika Mkoa huo wa Njombe.
Kabla ya kuhutubia mkutano wa hadhara, Rais Kikwete ambaye alikuwa katika siku ya pili ya ziara yake ya siku sita katika Mkoa wa Ruvuma, Rais Kikwete alikuwa na shughuli nyingi katika Wilaya ya Nyasa ambako amezindua Daraja la Ruhekei lililoko katika Kijiji cha Mkalole, kilomita nane kutoka mjini Mbamba Bay.
Alisema ujenzi wa daraja hilo ambalo lina sehemu tatu limejengwa kisasa kabisa ikiwa ni maandalizi ya ujenzi wa barabara ya lami kutoka Mbinga, Wilaya ya Mbinga kwenda Mbamba Bay, Wilaya ya Nyasa.
“Ni kweli Mwaka 2005 wakati wa kampeni ya Uchaguzi Mkuu nilishindwa kuvuka hapa kwa sababu daraja lilivunjika lakini ujenzi huu wa kisasa ni kwa sababu tunajiandaa kujenga barabara ya lami kuunganisha Mbinga na Mbamba Bay,” Rais Kikwete amewaambia wananchi kwenye daraja hilo.
Rais Kikwete pia ameweka jiwe la msingi la Ujenzi wa Makao Makuu ya Wilaya ya Nyasa katika Kijiji cha Kilosa kilichoko karibu na Mbamba Bay na amezindua usambazaji wa umeme katika vijiji vya Wilaya ya Nyasa. Rais Kikwete anaendelea na ziara yake mkoani Ruvuma.

 







Wednesday, July 23, 2014

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA AFUNGUA MKUTANO WA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA BRN


 Gavana  wa  Benki   Kuu  ya  Tanzania,  Prof.  Benno  Ndulu   akichangia   hoja   wakati  wa mkutano  wa  kupitia  taarifa  ya  mwaka mmoja ya utekelezaji  wa  Mpango  wa  Matokeo  Makubwa  sasa (BRN) uliofanyika  leo  Jumatano   Julai  23,  2014  katika  ukumbi   wa Mwalimu  Nyerere  Jijini  Dar es  Salaam.  Kulia  ni  Katibu   Mkuu  wa Wizara  ya Maji  na  Umwagiliaji  Mhandisi  Bashir Mrindoko

 

 katibu Mkuu  Kiongozi  Balozi   Ombeni  Sefue  akichangia  hoja  wakati mkutano wa kupitia taarifa  ya  mwaka  mmoja  ya  utekelezaji  wa Mpango wa Matokeo Makubwa sasa uliofanyika leo Jumatano   Julai  23,  2014  katika ukumbi   wa Mwalimu  Nyerere Jijini  Dar es  Salaam. Kulia  ni Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Asha- Rose  Migiro   na (katikati)  Mtendaji  Mkuu  wa  Ofisi  ya  Rais-  Usimamizi  wa  Utekelezaji  wa  Miradi  (PDB),  Bw. Omari Issa.






Naibu    Waziri  wa Viwanda  na Biashara, Mhe. Janet Mbene akichangia  hoja  wakati mkutano wa kupitia taarifa ya  mwaka  mmoja  ya  utekelezaji wa Mpango wa Matokeo Makubwa sasa uliofanyika leo Jumatano   Julai  23,  2014  katika ukumbi   wa Mwalimu  Nyerere Jijini  Dar es  Salaam. Kushoto  ni Katibu  Mkuu Ofisi  ya Waziri Mkuu Tawala  za  Mikoa  na Serikali  za Mitaa (TAMISEMI), Bw. Jumanne Sagini.
 
 
 
  Naibu  Waziri  wa  Katiba  na  Sheria, Mhe. Angellah Kairuki (katikati)  akichangia  hoja  wakati mkutano wa kupitia taarifa ya  mwaka  mmoja  ya  utekelezaji wa Mpango wa Matokeo Makubwa sasa uliofanyika leo Jumatano   Julai  23,  2014  katika ukumbi   wa Mwalimu  Nyerere Jijini  Dar es  Salaam.
 
 

 Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Harrison Mwakyembe  (kulia) akichangia akichangia  hoja  wakati mkutano wa kupitia taarifa ya  mwaka  mmoja  ya  utekelezaji wa Mpango wa Matokeo Makubwa sasa uliofanyika leo Jumatano   Julai  23,  2014  katika ukumbi   wa Mwalimu  Nyerere Jijini  Dar es  Salaam. Kutoka  kushoto  ni  Waziri  wa  Elimu na Mafunzo  ya Ufundi,  Mhe. Shukuru  Kawambwa,  Naibu  Waziri  wa Fedha  na Uchumi, Mhe.  Mwigulu Nchemba,  na Katibu  Mkuu wa  Wizara  ya Nishati  na Madini,  Eliakim Maswi.
(PICHA NA ISMAIL NGAYONGA- MAELEZO)

















Tuesday, July 22, 2014

HIVI NDIVYO VIUNGO VYA BINADAMU VILIVYOKUTWA KWENYE MFUKO USIKU HUU JIJINI DAR ES SALAAM

Jeshi la polisi Mkoa wa kipolisi Kinondoni, limefanikiwa kukamata viungo vya binadamu vikiwa kwenye mifuko ya plastiki katika maeneo ya Bunju eneo ambalo ni marufu kwa uchimbaji wa kokoto.


Viungo hivyo vilivyotambulika ni  kama vile miguu iliyokauka na mafuvu ya vichwa vya binadamu huku navyo vikiwa vimekaushwa.....
 
 
 
 
 
 
 Mmoja ya Kiungo cha Mguu
 
 
 
 
 
 
 
 
 Gari likiwa limebeba mifuko yenye viuongo hivyo, ambapo Jeshi la Polisi wilaya ya Kinondoni limesema kuwa limeanza uchunguzi wa kina baada ya kukakamata viungo mbalimbali vinavyodhaniwa kuwa ni vya binadamu katika  mifuko ya plastiki katika machimbo ya kokoto sehemu za Mbweni Mpiji, Magohe, nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.
 
 
 
Watu zaidi wakiwa wanaongezeka katika eneo la Tukio

Jeshi la Polisi wilaya ya Kinondoni limesema kuwa limekamata viungo mbalimbali vya binadamu vilivyohifadhiwa ktk mifuko ya plastiki ktk machimbo ya kokoto ya Bunju nje kidogo ya jiji la Dsm

Taarifa za tukio hilo zimethibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Camilius Wambura. 

Mpaka tunaondoka eneo la Tukio Miili ilikuwa imechukuliwa na Jeshi la Polisi kwa Uchunguzi zaidi, Taarifa kamili itatolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dar es salaam.





Endelea kufuatilia hapa tukio hili hapa blog.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

Popular Posts