Thursday, May 29, 2014

WAMILIKI WA MAGHOROFA IRINGA YANAYOJENGWA BILA VIBALI IRINGA KUBANWA

Wito umetolewa kwa watu wanaotaka kujenga majengo ya ghorofa kuhakikisha wanapata vibali vya kumruhusu kujenga majengo hayo kabla hajaanza kujenga na pia kuwa na ramani ya mchoro wa jengo analotaka kulijenga.
Akizungumza na mtandao huu wa www.matukiodaima.com ofisini kwake Mkaguzi Msaidizi wa Zimamoto na Uokoaji mkoani Iringa Ispekta Shomari Salla alisema kuwa jengo lolote linalojengwa kwa ajili ya biashara ni lazima likaguliwe ramani ya jengo hilo na kikosi cha zimamoto pamoja na mipango miji kabla halijaanza kujengwa.
“kanuni ya ukaguzi ya mwaka 2007 na hati ya mwaka 2008 ya zima zoto imeainishwa kuwa jengo la gorofa la aina yeyote ile ni lazima likaguliwe kabla ya kujengwa haijalishi lipo maeneo gani yawe ya mkusanyiko au sio ya mkusanyiko ni lazima ramani ya mchoro wa hilo jengo upelekwe kwa mipango miji waukague halafu uje kwetu pia tuukague kwanza ndipo tumruhusu huyo mtu aendelee na ujenzi wake na tutamruhusu tu endapo kama atakuwa ametimiza hayo masharti na pia kama sisi tutakuwa tumeridhishwa na vigezo alivyovileta kwetu tuviangalie, kama hatokuwa na hivyo vigezo basi hatuwezi kumruhusu kujenga jengo lolote lile” alisema Salla.
Hata hivyo aliwataka makandarasi kuwaruhusu na pia kuwapa ushirikiano watu wanaoenda kukagua gorofa ambalo litakuwa bado linajengwa, na kwa upande wa wamiliki wa majengo hayo watafute wakandarasi wenye ujuzi na uzoefu mzuri wa ujenzi ili majengo yao yajengwe kwa uimara zaidi na pia alitoa onyo kwa yeyote atakayekiuka masharti hayo na kujenga bila kibali basi hatua kali za kisheria zitachukuliwa.
 
NA DIANA BISANGAO WA MATUKIO DAIMA.COM, IRINGA

No comments:

Post a Comment

Popular Posts