Friday, September 5, 2014

DK. MAGUFULI AWATISHA WANANCHI KONGWA

WAZIRI wa Ujenzi Dk. John Magufuli na Rais Kikwete

WAZIRI wa Ujenzi Dk. John Magufuli, ametumia nafasi ya uwekaji wa jiwe la msingi katika barabara ya Mbande Kwangwa kuwatisha wananchi kuwa iwapo watachagua viongozi nje ya CCM watashidwa kufungua barabara hiyo.
Magufuli, alitoa kauli hiyo wakati akitoa utangulizi wa kumkaribisha Rais Jakaya Kikwete katika uzinduzi wa barabara ya Mbade Kongwa yenye urefu wa kilometa 5 zilizogharimu sh bilioni 2.9.
Alisema kuwa juhudi ambazo zinafanywa na serikali ya CCM za kuwajengea barabara wananchi wa maeneo mbalimbali ili kuhakikisha wanarahisisha uchumi wao.
“Leo wananchi wa Kongwa nataka niwaambie kuwa, tunaweka jiwe la msingi na nataka kuwahakikishia kuwa barabara hii itafunguliwa na wewe Rais Kikwete kabla hujamaliza muda wako, pia ni lazima tumalize ujenzi wa barabara yote yenye urefu wa kilometa 101.1.
“Nataka niwaambie watani zangu Wagogo, mkiweka madarakani mtu kutoka nje ya CCM, kuna uwezekano mkubwa akaja kufungua kipande hiki cha kilometa tano tu na kwingine akapaacha bila kupajenga, sasa nataka niwaambie mkifanya mchezo mwafaaa… lakini sipigi kampeni,” alisema Dk Magufuli.
Kwa upande wake, Rais Kikwete alisema kuwa ni aibu kwa nchi kama Tanzania, kuendelea kuomba omba kwa wafadhili kwa ajili ya ujenzi wa barabara.
Chanzo;Tanzania Daima 

No comments:

Post a Comment

Popular Posts