Thursday, September 25, 2014

SHIRIKA LA KAZI DUNIANI (ILO) LATOA ELIMU YA MAAMBUKIZI YA UKIMWI KWA WATUMISHI WA UMMA.

Shirika la kazi duniani kushirikiana na Ofisi ya Rais Sekretalieti ya Utumishi wa Umma imezindua elimu ya kujinginga na maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi kwa watumishi wa umma katika mkoa wa Njombe,uzinduzi huo ulifanyika katika ukumbi wa Halmashuri ya Njombe na ulizinduliwa na katibu Mkuu utumishi Bwan. Gorgeg Yambesi.
Katibu Mkuu aliwataka watumishi kujitokeza na kupima afya zao ili kujitambua mapema na serikali iweze kuwasidia,kwa kuwawezesha kwa kuwapa huduma bora ili waweze kufanya kazi kwa amani na ufanisi.
Yambes alisema kuwa uzinduzi  huwo wa kupima maambukizi ya UKIMWI kwa hiari kwa watumishi  umefanyika katika Mkoa wa Njombe kutoka na Mkoa huo kuwa na kuongoza kwa Maambukizi.

Naye Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Njombe ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Njombe Bibi Salara Dumba alisema kuwa Mkoa wa Njombe unaongoza kwa maambukizi ya Ukimwi kwa asilimi 14.8 na kufutiwa na Iringa asilimia 9.1.
Dumba alisema Mkoa wa Njombe unaongoza kwa maambukizi kutoka na Mila potofu kama vile kurithishana wajane,kutakasa wagane na wanaume kutofanya tohara.
Naye mwakislishi wa Shirika la kazi Duniani Bibi Getrudi Sime alisema shirika hilo limelidhia Mkataba wa mwaka 2010 kwa kutambua kuwa VVU na UKIMWI una athari kubwa kwa jamii na uchumi kwa ulimwengu wa kazi katika sekta  rasmi na zisizo rasmi.










No comments:

Post a Comment

Popular Posts