Monday, July 6, 2015

Dr Shein Apitishwa Kuwa Mgombea Urais wa Zanzibar

 


Kamati kuu maalum ya chama cha mapinduzi Zanzibar kwa kauli moja imempitisha Dr Ali Mohamed Shein kuwa mgombea urais wa Zanzibar kupitia chama cha mapinduzi.
 
Hatua hiyo imefikiwa baada ya wajumbe wa NEC wa Zanzibar wanounda kamati maalum ya Zanzibar kukutana hapa Zanzibar katika ofisi kuu ya CCM na kuamua kumuidhinisha Dr Shein kugombea tena  kiti hicho cha urais baada ya wajumbe karibu 102  ambao ni aslimia 83  kuridhia Dr Shein agombee.
Awali Dr Shein ambaye ni makamu mwenyekiti wa CCM Zanzibar alilazimika kuondoka ndani ya kikao ili ijadaliwe na wanachama hao ambapo kiti hicho kilishikwa kwa muda na Dr Mohamed Gahribu Bilali makamu wa rais, ambapo baadaye akizumgumza na wanaccm hao waliokubali Dr Shein aliwahidi wanachama wa CCM kuwa  uamuzi wake uko palepale wa kutekeleza ilani ya CCM ya kuitumikia Zanzibar.
Katika hatua nyengine naibu katibu mkuu wa CCM Zanzibar akizungumza baada ya kikao hicho alisema CCM haiwezi kupinga au kukubali suala la majimbo,wao wanasubiri maamuzi ya tume na wako tayari kwa umauzi wowote utakaotolewa na tume ya uchaguzi ambayo inatarajiwa kutangaza majimbo mapya leo asubuhi.
Kupitishwa kwa Dr Shein kugombea urais wa Zanzibar na kamati maalum ni hatua ya kwanza na sasa shuguhli yote inahamia Dodoma ambapo jina la Dr Shein litajadiliwa na kamati kuu na baadaye kutakiwa kuidhinishwa na kupitishwa na halmashuri kuu ya CCM, nafasi ya urais wa Zanzibar inaamuliwa na NEC na siyo na mkutano mkuu waccm.

EDSONI KAMUKARA PUMZIKA KWA AMANI













 Edson Slavatory Kamukara, amezikwa kijijini kwao Ihangiro wilayaniMuleba, huku akiacha majonzi kwa familia yake, baada ya kuacha mtoto mmoja ilhali mama yake akisumbuliwa na kupooza, ambapo siku chache zilizopita, Edson alitokea Muleba kumuangalia mama yake, kama alivyozungumza dada wa marehemu aliyejulikana kwa jina la Joyce.


 Akizungumza katika maziko hayo, mkurugenzi wa kampuni ya mwana halisi publishers LTD Bwana Said Kubenea, amesema kifo cha marehemu Kamukara, kimezua utata kutokana na hakuna anayejua undani,
huku akisema kuwa madakatari wanasema inaonekana alikufa baada ya kukosa hewa huku, chumbani kwake kukikutwa na damu, akiongeza kuwa alikuwa anakamilisha kazi ya uandishi uliokuwa ukiwahusu vigogo na kama habari zake zingetoka, saizi nchi ingekuwa inaongea mambo mengine.




Waadishi kutoka chama cha waandishi  habari mkoani Kagera KPC, walishiriki maziko hayo na ndiyo walihusika kubeba mwili wa marehemu na picha chini ni Charles Mwebeya akitroa rambirambi yao kwao dada Joyce ambaye anaishi Dar na alikuwa karibu na marehemu














 Marehemu Edson Kamukara, ameacha mtoto anakadiriwa kuwa na miaka kati ya 3 hadi 4 aitwaye  Edigar Ishengoma, na marehemu alianzia kazi ya uandishi katika gazeti la Majira, akafanya jambo leo, tanzania dai, na hatimaye mwanahalisi publishers ambapo amefanyia kwa kipindi cha miezi minne, na alikuwa anakamilisha habari kuhusu matatizo ya wananchi kupitia viongozi mkoani Kagera.
Na Mwanaharakati.







MWENGE WAZINDUA MIRADI YA THAMANI YASHILINGI BILIONI KUMI NA TATU NJOMBE



Miradi ya Shilingi billion Kumi na  tatu (13,201,109,235.55) inatalajiwa kuzinduliwa,kuwekewa jiwe la Msingi na kukaguliwa na mbio za Mwenge wa Uhuru katika Mkoa wa Njombe,hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Njombe  Dk.Rehema Nchimbi wakati akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka Mkoa wa Iringa.
Nchimbi alisema kuwa Mwenge wa Uhuru katika Mkoa wa Njombe utakimbizwa katika halmashauri Sita ambazo ni Njombe,Makete,Ludewa,Wanging’ombe,Mji Njombe  na Mji Makambako,Katika halmashuri jumla ya
Miradi 45 itatembelewa na Mwenge wa Uhuru.
Alisema kuwa Miradi hiyo ipo katika sekta ya Afya ,Elimu,Kilimo,Miundombinu,Utalii na Misitu,miradi mingi imekamilika na kuanza kutumika .
Naye mkimbiza Mwenge Kitaifa  Juma Khatibu chum alisema kuwa amefurai kuingia Mkoa wa Njombe  na anarajia kufungua,kukagua miradi mizuri kwani kutokana na mapokezi walioyapata ya wananchi wengi  waliojitokeza kuupokea Mwenge wa Uhuru, Kauli mbiu ya Mwenge Mwaka huu ni “Tumia haki yako kidemokrasia ,Jiandikishe  na kupiiga kura katika uchaguzi wa mwaka 2015.




Wednesday, June 24, 2015

Dkt. Nchimbi atangaza rasmi kutogombea Songea



Katika hali isiyokuwa ya kawaida baadhi ya wananchi wakiwemo wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) jimbo la Songea mjini mkoani Ruvuma, wamejikuta katika hali ya sintofahamu huku wengine wakimwaga machozi baada ya mbunge wa jimbo hilo, mh. Dkt. Emmanuel Nchimbi kutangaza rasmi kutogombea tena ubunge katika jimbo hilo.
Katika uwanja huu wa majimaji mjini songea, mbunge wa jimbo la Songea mjini, mh. Dkt. Emmanuel Nchimbi aliyelitumikia jimbo hilo kwa miaka 10 akakutana na wanachama wa chama cha mapinduzi pamoja na kuelezea mafanikio mbalimbali ya maendeleo aliyoyafanya katika jimbo hilo ikiwemo ujenzi wa barabara, zahanati na shule za sekondari lakini pia akatumia nafasi hiyo kutangaza rasmi kutogombea tena ubunge katika jimbo la songea mjini.
Tamko hilo la dkt. Nchimbi likazua simanzi kwa baadhi ya wananchi na wanachama wa CCM hapa Songea huku wengine wakishindwa kujizuia na kujikuta wakimwaga machozi.
Katika maelezo yao wanachama hawa wanasema kuachia ngazi kwa Dkt, Nchimbi kutogombea katika jimbo hilo kunatoa fursa kubwa kwa vyama vya upinzani kuchukua jimbo hilo hali ambayo hawakubaliani nayo.
Hata hivyo wanachama hao wakamuomba mbunge huyo kutengua msimamo wake na kumtaka arejee tena kugombea jimbo la Songea mjini, jibu la dkt. Nchimbi ikawa anaenda kufikiria.







Shirikisho la Soka Tanzania(TFF) limemteua Charles Boniface Mkwassa, kuwa kocha mpya wa Timu ya Taifa ya Soka ya Tanzania(Taifa Stars)







Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania - TFF, Jamal Malinzi leo ameagana rasmi na aliyekua kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager, mholanzi Mart Nooij.

Akiongea na waandishi wa habari leo katika hoteli ya Tansoma, Malinzi amesema wameamua kuagana nae mbele ya vyombo ya habari kama iliyofanyika pia wakati wa utambulisho wake wakati wa kuanza kazi.

“Mpira wa miguu unachangamoto nyingi, watanzania tunasafari ndefu katika mafanikio ndio maana TFF imeanza kuwekeza katika soka la vijana, sababu ndio msingi wa kuwa na timu bora ya Taifa” alisema Malinzi.

Duniani kote chimbuko la timu bora ni soka la vijana na watoto, tukiwa na vijana wengi walioanza kucheza mpira katika umri mdogo wanapofikia umri wa kuchezea timu ya Taifa tutakua na kikosi bora.

Nchi za wenzetu inapofikia kocha kuita wachezaji wa timu ya Taifa anakuwa na wigo mpana, kwetu sisi wachezaji wanocheza soka nje ya nchi wanahesabika, hivyo ni lazima tuanze kuwekeza kwenye soka la vijana.

TFF ilishaanza mkakati huo ndio maana kuna timu za U13, U15 ambazo zitakua zikiingia kambini na kucheza michezo ya kirafiki ndani ya nje kwa lengo la kupata uzoefu kabla ya kushiriki kuwania kufuzu kwa fainali za vijana mwaka 2016.

Kikosi cha U15 kinatarajiwa kufanya ziara mwezi Disemba mwaka huu katika nchi za Malawi, Zambia, Zimbambwe, Botswana na Afrika Kusini, kisha mwakani mwezi April 2016 kitaenda Rwanda, Burundi, Uganda na Kenya kucheza michezo ya kirafiki.

Naye Mart Nooij aliyekua kocha wa Taifa Stars, akiongea na waaandishi wa habari alisema anawashukuru watanzania wote, serikali, wadau wa mpira wa miguu nchini na TFF kwa sapoti waliyompatia wakati akiwa kocha mkuu wa timu ya Taifa.

Nooij alisema alifurahia maisha yake akiwa Tanzania kwa kipindi chote alichokua akifundisha timu ya Taifa, lakini kwa sababu imefikia mwisho wa ajira yake hana jinsi anaondoka, lakini ataendelea kuikumbuka Tanzania na watanzania wote kila siku kwa ukarimu wao.

Wakati huo huo Rais wa TFF. Jamal Malinzi amemtangaza Charles Mkwasa kuwa kocha mpya wa Taifa Stars akisaidiwa na kocha Hemed Morocco, Mkwasa ambaye ni kocha wa Yanga na Morocco kocha wa Mafunzo watafanya kazi kwa kipindi cha miezi mitatu ambayo timu ya taifa itakua na michezo ya kuwania kufuzu kwa CHAN na AFCON.

Malinzi amesema uteuzi wa makocha hao wazawa umezingatia vigezo vya makocha wa timu ya Taifa kuwa na leseni A ya ukocha kutoka CAF au zinazofanana kutoka mashiriksho mengine duniani wanaozifanyia kazi, jambo ambalo makocha hao wazawa wamekizi.

Kocha Mkwasa atakua akipewa hudumu zote na masilahi (zikiwemo posho) alizokuwa anapewa kocha aliyeondoka, pia amepewa nafasi ya kuchagua benchi lake la ufundi la kufanya nalo kazi, hivyo nawaomba wadau wa mpira wa miguu na watanzania kwa ujumla tuwape sapoti makocha hao wazawa” aliongeza Malinzi”

Aidha Kamati ya utendaji ya TFF Iimemteua Alhaj Ahmed Mgoyi kuwa mratibu wa timu ya Taifa, lengo la uteuzi huo wa Mgoyi ni kuwa kiunganishi kati ya kamati ya Utendaji na timu ya Taifa.

U15 Yaingia  Kambini
Timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 15 ya Tanzania, imeingia kambini jana na kuanza mazoezi leo katika uwanja wa Karume kujiandaa na mchezo wa kirafiki dhidi ya kombaini U15 ya mkoa wa Mbeya siku ya jumapili.

Kikosi hicho kilicho chini ya makocha Bakari Shime na Peter Manyika kitacheza mchezo huo kwa lengo la waalimu kupatawa fursa ya kuwaona vijana hao na kuwaongeza wengine watakaoneka katika kikosi hicho.

U15 ni mpango wa TFF kuandaa kikosi kizuri chenye ubora kuelekea kuwania kufuzu ka fainali za vijana Afrika mwaka 2017 zitakazofanyika nchini Madagascar, ambapo vijana hao watakua na umri wa miaka 16 kufikia mwakani wakati michezo ya kuwania kufuzu itakaponza mwezi Julai, 2016.

NB: Kesho siku ya jumatano kocha mpya wa Taifa Stars, Charles Mkwasa na msaidizi wake Hemed Moroco wataongea na waandishi wa habari saa 5:30 asubuhi katika ukumbi wa mikutano wa TFF uliopo Karume.

Waandishi wote wa habari mnaombwa kuhudhuria bila kukosa.

Imetolewa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania

Mjamzito Afanyiwa Ukatili wa Kutisha



 MJAMZITO aliyefahamika kwa jina la Rotha Bujiku, amejifungulia bafuni karibu na zahanati ya kijiji baada ya kudaiwa kufukuzwa na wauguzi waliokuwa zamu siku hiyo, kwa maelezo kuwa anajifungua kila mwaka.
 
Tukio hilo lilitokea wilaya ya Maswa katika mkoa wa Simiyu majira ya saa 2 asubuhi baada ya mjamzito huyo kufika katika zahanati hiyo kwa lengo la kupata huduma ya kujifungulia kwa wataalamu.
 
Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo lililovuta umati wa watu, mjamzito huyo alikataliwa kupokewa na muuguzi wa zamu aliyetajwa kwa jina la Constansia John.
 
Ilielezwa kuwa muuguzi huyo alikataa kumpokea kwa madai kuwa mjamzito huyo alishapewa maelekezo tangu awali kuwa anatakiwa akajifungue katika hospitali ya wilaya ya Maswa kwani amekuwa akizaa watoto kwa mfululizo.
 
Inaelezwa kwamba, wakati Rotha akiugulia maumivu ya uchungu, muuguzi huyo alimpigia simu ya mkononi Muuguzi Mkunga wa zahanati hiyo, Leticia Kachumi kumjulisha hali hiyo na alipofika alitaka mjamzito huyo aondoke katika eneo hilo na atafute usafiri ili aweze kufika katika hospitali ya wilaya kama alivyoelekezwa katika siku za nyuma.
 
“Leticia alipofika hapo zahanati baada ya kupigiwa simu na Constansia, licha ya kumuona anaendelea kulalamika kutokana na uchungu alimwamuru aondoke eneo hilo mara moja na atafute usafiri wa kumfikisha hospitali ya wilaya iliyoko umbali wa kilomita 36, kwani walishamweleza kuwa amekuwa akizaa mfululizo na hiyo ni mimba ya kumi na moja,” alisema shuhuda, Kundi Mageni.
 
Kutokana na hali hiyo, mjamzito huyo alilazimika kuondoka zahanati hapo bila msaada wowote na baada kufika karibu na nyumba iliyoko na zahanati hiyo, alikwenda katika bafu la nyumba ya jirani ambalo halina sakafu na kujifungulia humo na baadaye kusaidiwa na wasamaria wema waliosikia sauti ya mtoto.
 
“Kwa kweli huyu mama amejifungulia katika mazingira machafu na hatarishi kwa afya yake na mtoto aliyemzaa. Kwa kweli hili ni tukio la kusikitisha. Huwezi kuamini wauuguzi hao ambao ni wanawake kumtendea mwenzao ukatili wa kiasi hiki,” alisema Pili Kidesela, Diwani wa kata ya Shishiyu (CCM).
 
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dk Jonathan Budenu aliyefika katika eneo la tukio muda mfupi baada ya kupata taarifa hizo, alisema kitendo kilichofanywa na wauguzi hao ni kinyume cha maadili ya kazi yao na hivyo ni lazima hatua kali za kinidhamu zichukuliwe kwa wote waliohusika.
 
Mwingine ajifungulia kichakani 
Wakati hayo yakitokea Maswa, mkoani Arusha binti mwenye umri wa miaka 17 alijikuta akijifungulia kichakani baada ya kuzidiwa uchungu wakati akisubiri kuombewa kwenye mkutano wa dini uliofanyika Viwanja vya Magereza, Kisongo nje kidogo na Jiji la Arusha.
 
Anna Ngitoria, mkazi wa Endurimeti, wilayani Arumeru, alikuwa miongoni mwa mamia ya wakazi wa Arusha, Kilimanjaro na vitongoji vyake waliokuwa wamekusanyika kwa wingi kwenye uwanja huo wa magereza kwa ajili ya kile kilichodaiwa kuwa ni maombi yaliyoandaliwa na kituo kimoja cha redio cha jijini Arusha, Radio Safina.
 
Kwa kawaida uongozi wa kituo hicho huandaa makongamano ya kila mwezi kwenye uwanja huo wa Kisongo na kujumuisha mamia ya watu, wengi wao wakiwa ni wanawake na wasichana ambao hupendelea kuhudhuria maombezi hayo kwa matarajio tofauti.
 
Mikusanyiko ya maombi ya ‘Radio Safina’ imekuwa ikikusanya watu wengi mithili ya ‘Kikombe cha Babu,’ ambacho nacho kilivuma sana miaka mitatu iliyopita na tukio la msichana huyo kujifungua katika moja ya matukio hayo kimezua hisia tofauti mjini hapa.
 
Akizungumza katika hospitali ya Mount Meru ambapo amelazwa kwa sasa, binti huyo, Anna amekiri kuwa alijifungua kabla ya wakati kwa sababu alikuwa na ujauzito wa miezi saba tu.
 
Mtoto wake njiti sasa anahudumiwa katika wodi maalumu iliyopo hospitalini hapo na wauguzi wanasema anaendelea vizuri.
Mpekuzi blog

TANZIA: Mbunge wa Geita, Donald Max afariki Dunia.



 Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Geita (CCM) Mheshimiwa Donald Kevin Max (58)(picha) amefariki dunia.

Kufuatia taarifa iliyotolewa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Anne Makinda (Mb) kwa Waheshimiwa Wabunge wote pamoja na umma kwa ujumla, Mhe. Max amefariki dunia tarehe 23 Juni, 2015 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alikokuwa akipatiwa matibabu.

Kwa mujibu wa taarifa hii, taarifa zaidi juu ya msiba huu zitaendelea kutolewa na Ofisi ya Bunge kwa kushirikiana na familia kadri zitakavyopatikana ikiwa ni pamoja na ratiba ya Mazishi.

“BWANA ametoa, BWANA ametwaa,
Jina la BWANA lihimidiwe.” Amina.

Imetolewa na:
Ofisi ya Bunge,
Idara ya Habari, Elimu kwa Umma na
Uhusiano wa Kimataifa,

DODOMA

Urais CCM: Waliorudisha Fomu ya Urais

WIKI moja kabla ya kwisha kwa muda wa warudisha fomu kwa makada wa CCM waliojitokeza kuwania kupitishwa na chama hicho kuwania urais wa Tanzania, ni wanachama sita tu kati ya 39 ndio waliorudisha fomu mpaka sasa.
 
Kwa mujibu wa ratiba ya mchakato wa kumpata mgombea wa urais ndani ya CCM, mwisho wa kurudisha fomu ni Julai 2, mwaka huu ambapo kila aliyechukua fomu anatakiwa kuwa na wadhamini 450 kutoka mikoa 15 ambapo mitatu iwe ya Zanzibar.
 
Idadi ya wanachama waliojitokeza mwaka huu inaonekana kuwa ni kubwa, mara tatu zaidi ya waliojitokeza mwaka 2005 ambapo wagombea walikuwa 11, ingawa Rais Jakaya Kikwete ndiye aliyeibuka kidedea na kutetea tena ushindi wake mwaka 2010.
 
Waliorudisha fomu ni Waziri wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal, Makongoro Nyerere (Mbunge wa Afrika Mashariki), Waziri wa Ujenzi Dk John Magufuli, Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Steven Wassira na Balozi Ally Karume.
 
Wengine waliojitokeza kuchukua fomu ni Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, Mawaziri wakuu wa zamani, Frederick Sumaye na Edward Lowassa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalumu), Profesa Mark Mwandosya na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe.
 
Pia wamo Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, Naibu Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia, January Makamba, Mbunge waSengerema, William Ngeleja, Mkazi wa Musoma mkoani Mara, Boniface Ndengo na mkulima kutoka Kijiji cha Mjimtala Wilaya ya Kasulu, Kigoma, Idelphonce Bilohe na Balozi Augustino Mahiga.
 
Wengine ni Dk Hans Kitime, Dk Mwele Malecela, Mbunge wa Nzega Dk Hamis Kingwangala, Balozi Amina Salum Ally, Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba, Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina, Mtumishi wa CCM, Amos Siyantemi, Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta, Wakili Mwandamizi Godwin Mwapongo, Peter Nyalile, Leonce Mulenda, Jaji Mkuu Mstaafu, Augustino Ramadhani na Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Asha-Rose Migiro.
 
WanaCCM wengine wanaoutaka Urais ni Prof. Sospeter Muhongo, Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk Titus Kamani, Monica Mbega, Patrick Chokala, Joseph Chagama, Malick Malupu, Ritha Ngowi na mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Amos Robert.
Mpekuzi blog

Tuesday, June 23, 2015

Nape: CCM itashinda tu hata kwa goli la mkono









 CCM imesema kuwa itahakikisha inarudi Ikulu hata “kwa bao la mkono” wakati wa Uchaguzi Mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba 25.

Katibu wa itikadi na uenezi wa chama hicho, Nape Nnauye alisema hayo katika mkutano wa hadhara uliofanyika jana kwenye viwanja vya Nyehunge wilayani hapa.

Neno “bao la mkono” hutumiwa kama goli lililofungwa kwa kuupiga mpira kwa mkono kinyume cha taratibu za mpira, lakini hukubaliwa kwa kuwa mwamuzi anakuwa hajaona kitendo hicho.

“Rangi inayoenda Ikulu ni hii (anaonyesha shati lake la kijani ambayo hutumiwa na chama hicho). Tuna uhakika na ushindi wa Rais. Kwa namna yoyote ile, CCM itarudi Ikulu hata kama ni kwa bao la mkono... bao ni bao tu ili mradi refa hajaona,” alisema Nape.

Nape, aliye kwenye ziara ya katibu mkuu wa CCM, aliwataka wananchi wa Sengerema kusubiri ushindi wa chama hicho na kuwakumbusha kuwa wanapaswa kuiweka CCM kuanzia udiwani mpaka ubunge kwa nafasi ya urais tayari kuna uhakika.

Katika mkutano huo, Nape alisema ana uhakika CCM itashinda baada ya kushuhudia mwitikio wa Watanzania tangu alipoanza kuongozana na Kinana katika ziara zake za kuizunguka nchi na kuzungumza na wananchi pamoja na kusikiliza kero zao.

Amebainisha kuwa amejifunza na kujiridhisha kuwa chama chake bado kinapendwa miongoni mwa wapigakura waliofikiwa tofauti na vyama vya upinzani.

“Tumefika maeneo mengi ambayo upinzani haujafika. Huko tuna hazina kubwa ya wanachama. Hakuna namna Ukawa wanaweza kuingia Ikulu mwaka huu,” alisisitiza.

Wapinzani waja juu
Kauli hiyo ya Nape ilipingwa na viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani waliosema kuwa mtendaji huyo anamaanisha kuwa CCM itaiba kura.

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa hakutaka kabisa kuzungumzia kauli ya Nape zaidi ya kusema watakutana Oktoba.

“Kwa bahati mbaya kauli za Nape siwezi kuzijibu. Kauli za Nape zichukue kama zilivyo, ingekuwa ni (katibu mkuu wa CCM, Abdulraham) Kinana, ningemjibu lakini ajue kuwa tutakutana Oktoba,” alisema Dk Slaa alipoulizwa na Mwananchi kuhusu suala hilo.

Naibu mkurugenzi wa habari wa CUF, Abdul Kambaya alisema kauli ya Nape inamaanisha kuwa CCM itaiba kura kwani kwa kawaida bao la mkono ni bao haramu.

“Kauli hiyo inaonyesha dhahiri kuwa wataiba kura na kwa sababu katiba yetu ni mbovu matokeo yake yatatangazwa kama yalivyo… hiyo ndiyo maana ya bao la mkono,” alisema.

Kambaya alisema hata hivyo CCM isijiaminishe kwa lolote kwani hivi sasa wananchi wamebadilika kimtazamo kutokana na matatizo mengi yanayoiandama nchi kama vile afya, elimu duni na migogoro ya ardhi.

“Lakini CCM wajue kuwa kutatokea machafuko makubwa iwapo wamejipanga kuingia Ikulu kwa njia hiyo ya bao la mkono. Kauli ya Nape ni ya kidikteta na inaonyesha dhahiri kuwa wamejikita kwenye utawala wa mabavu,” alisema.

Kadhalika Kambaya alisema CUF imeshajipanga na kuhakikisha inaziba mianya yoyote ya wizi wa kura kuanzia kwenye Daftari la Wapigakura hadi katika ujanja wa kuwapigisha kura marehemu, askari na wanajeshi kama inavyodaiwa kufanyika Zanzibar.

Katibu mkuu wa NCCR-Mageuzi, Mosena Nyambabe alisema Nape anatoa maneno ya kuvutia kwake kama njia ya kuwakatisha tamaa wapinzani na wanachama, hata hivyo alimuonya kuwa siasa za sasa hazitabiriki kwa njia hiyo.

“Lakini ajue kuwa mambo yanabadilika. Anaweza kushangaa mambo yakawa mengine, sasa hivi wananchi wana mwamko mkubwa na wanabadilika,” alisema.

Alisema CCM haina haja ya kujitapa kwa sasa wakati bado haijapata mgombea kwani huenda wakapata ambaye wananchi hawatamuunga mkono hata kidogo.

“Bado CCM wana makundi jambo ambalo kwao ni udhaifu. Lakini pia lazima wajue kuwa wakati wa mchujo utakapofika, wale watakaokatwa hawatafurahia kuachwa na hapo kuna sababu za wapinzani kushinda,”alisema.

Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia alisema wakati Nape anabishana kwenye majukwaa, NCCR inaendelea kupiga kazi.

“Badala ya kujadili hoja za msingi zenye manufaa kwa wananchi yeye anajadili CCM kupiga bao?” alihoji Mbatia.

Akijibu hoja ya Nape, Naibu Katibu Mkuu wa TLP, Nancy Mrikaria alisema kauli ya kada huyo imekaa kisiasa na si kiuhalisia kwani ni kawaida kwa chama cha siasa kujiaminisha kuwa kitashika dola.

“Unajua chama chochote hata kiwe kidogo lazima kikiri kuwa kitashika dola ili mradi ilani yao inakubalika na unakubaliwa na wananchi kwa sababu chama chochote nia yake ni kuingia ikulu,” alisema.

Alisema hata vyama vidogo kama TLP hukiri ushindi kwa kusema kuwa vinataka kuingia ikulu kwa sababu chama hakiwezi kukiri mbele ya wananchi kuwa hakitashinda.
source Mpekuzi
















Serikali yakana kumtorosha Rais wa Sudani






 Serikali ya Afrika Kusini imekana ripoti kwamba mawaziri wake walipanga njama ya kumtorosha rais wa Sudan Omar El Bashir wiki iliopita.
 
Katika tukio hilo nusura rais huyo akamatwe kufuatia agizo la mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu wa kivita dhidi yake kutokana na mashtaka ya mauaji ya kimbari.
 
Mahakama ya Afrika Kusini ilimuagiza Bashir kusalia nchini humo huku ikijadiliana kuhusu iwapo agizo hilo litekelezwe. Lakini kabla ya mahakama hiyo kutoa uamuzi wake bwana Bashir aliondoka nchini Afrika Kusini na kurudi nyumbani.
 
Rais huyo wa Sudan alikuwa nchini Afrika Kusini kwa mkutano wa viongozi wa bara Afrika na kwamba serikali ilikuwa inajua kwamba ilihitajika kumkamata kwa kuwa mwanachama wa ICC.
 
Kwa mujibu wa  gazeti la Sunday Times nchini Afrika Kusini limenukuu duru za serikali kwamba katika mkutano wa mawaziri ilikubalika kwamba Afrika Kusini itamlinda hata iwapo italazimika kukiuka uamuzi wa mahakama na kukiuka katiba.
 
Katika taarifa yake,serikali imekana kwamba kulikuwa na mkutano wa siri na kwamba itaipatia mahakama hiyo maelezo kuhusu vile Bashir alivyoondoka nchini humo.
 
Mahakama kuu imeipatia serikali ya taifa hilo hadi alhamisi kubaini ni vipi aliruhusiwa kuondoka.

Ngassa arejea Yanga kiaina








Mshambuliaji wa Free Stars ya Afrika Kusini,Mrisho Ngassa (kulia) akifanya mazoezi na timu yake ya zamani Yanga baada ya kurejea nyumbani kwa mapumziko kwenye uwanja wa karume Dar es Salaam Jana.Picha na Said Khamis. 



Dar er Salaam. Mshambuliaji Mrisho Ngassa aliyesajiliwa na klabu ya Free State Stars ya Afrika Kusini hivi karibuni, jana aliibuka katika mazoezi ya timu yake ya zamani Yanga.
Ngassa alisajiliwa na Free State Stars kwa mkataba wa miaka minne mwishoni mwa mwezi uliopita na alirudi nchini kwa ajili ya kuitumikia Taifa Starsiliyokuwa ikicheza dhidi ya Uganda katika mechi ya kuwania kufuzu kushiriki fainali za Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani (CHAN), ingawa Shirikisho la Soka Afrika (CAF) lilimzuia kwani ameishasajiliwa nje ya ligi ya Tanzania.
Gazeti hili lilimshuhudia mshambuliaji huyo akifanya mazoezi na Yanga mwanzo mwisho na alipomaliza mashabiki wa klabu hiyo walilisukuma gari lake mpaka nje geti wakionyesha mapenzi kwa mchezaji huyo.
Ngassa ameitumikia Yanga kwa mafanikio kabla ya kuamua kuachana nayo na kwenda kusaka ulaji katika klabu ya Free State.
Ngassa alisema ameamua kufanya mazoezi na Yanga kwani bado iko moyoni mwake na hakuondoka kwa ubaya.
“Hapa kama niko nyumbani, kwani hii ni timu iliyo moyoni mwangu hivyo kama niko Dar es Salaam sioni ubaya kufanya mazoezi na Yanga kwani naamini kuna siku nitarudi hapa,”alisema Ngassa.
“Najiweka fiti wakati nikisubiri klabu yangu initumie tiketi ya kurudi Afrika Kusini maana walinipa ruhusa ya kuja Dar es Salaam kwa ajili ya timu ya Taifa, lakini nikazuiwa kucheza mechi na Uganda,” alisema Ngassa.
Msimu uliopita haukuwa mzuri kwa Ngassa kwani aliifungia Yanga mabao manne tu licha ya kuchaguliwa kuwa mchezaji bora wa Aprili

















Urais 2015: Mwanamke wa 5 ajitosa kuchukua fomu CCM



















 Mwananmke mwingine  ambaye ni kada wa CCM, Ritta Ngowi amechukua fomu ya kuomba kuteuliwa na chama kuwania urais katika uchaguzi utakaofanyika Oktoba mwaka huu.
 
Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu jana makao makuu ya CCM mkoani Dodoma Ngowi alisema akifanikiwa kuwa rais  ataanzisha kituo kikubwa cha kuwahudumia wastaafu, walemavu, wasiojiweza na vijana.
 
Kingine atakachofanya ni kuendeleza mazuri yaliyofanywa na marais waliopita, lakini zaidi akiweka mkazo kwenye masuala ya elimu na kukuza uchumi.
 
Aidha Ritha anafanya ,  idadi ya wanawake waliojitosa mbio za urais kufikia watano kati ya 39 waliochukua fomu hadi sasa.
 
Wanawake wengine ni Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Asha-Rose Migiro, Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa (NIMR), Dk Mwele Malecela, Balozi Amina Salum Alli na Monica Mbega.

Kocha wa Taifa Stars Maart Nooij na Benchi Lake Lote La Ufundi Watimuliwa Kazi




 Kocha Mkuu wa Taifa Stars Maart Nooij akisindikizwa na ulinzi mkali usiku wa kuamkia leo baada ya kumalizika kwa mchezo wa Tanzania na Uganda wa kuwania kufuzu fainali za CHAN katika Uwanja wa Amaan mjini Zanzibar ambapo Taifa Stars ilichapwa 3-0. *******
Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) katika kikao chake cha leo pamoja na mambo mengine kilipitia mwenendo wa timu ya Taifa (Taifa Stars) ikiwa ni pamoja na kuhudhuria mchezo kati ya Tanzania na Uganda, kama sehemu ya tathmini ya mwenendo wa timu.
 
Kamati ya Utendaji kwa kauli moja imeamua yafuatayo;
1. Ajira ya Kocha Mkuu Maart Nooij inasitishwa mara moja kuanzia Juni 21, 2015.
 
2. Benchi lote la ufundi la Taifa Stars limevunjwa kuanzia Juni 21, 2015.
 
3. Uongozi wa TFF utatangaza punde benchi jipya la ufundi la timu ya Taifa.

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA 
MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
Juni 20, 2015















Monday, June 22, 2015

Lowassa Azidi Kupata Mapokezi Makubwa

WAZIRI Mkuu Mstaafu,Edward Lowassa amesema hana shaka na swala la kukatwa jina lake katika vikao vya Chama cha Mapinduzi(CCM), kwani anaamini Chama chao kitatenda haki kwa kurudisha jina lake kuwa mgombea urais wa Tanzania.

Lowassa aliyasema hayo jana wakati akizungumza na wanachama wa CCM na wananchi wa Mkoa wa Ruvuma katika ofisi kuu za CCM Mkoani humo, wakati akitoa shukrani baada ya kudhaminini na wanaCCM zaidi ya elfu 52.

"Nimekuwa mwanaCCM tangu mwaka 1977 nilipomaliza chuo kikuu, sijawahi kufanya kazi nje ya CCM hivyo nakijua chama na hakuna mgombea atakayeweza kuvunja rekodi ya utendaji wangu katika chama, sasa leo anayetaka kukata jina langu anatoka wapi? anakata kwa sababu gani? Sioni kosa la kukatwa jina na Watanzania hawaoni, kwa hiyo msiwe na wasiwasi jina litarudi tu". alisema Lowassa.

Lowassa aliwasili Mkoani Ruvuma mapema  jana mchana akitokea Mkoani Iringa kwaajili ya kusaka wadhamini katika mbio zake za kusaka urais kwa tiketi ya chama hicho, ambapo umati wa watu ulifurika kumlaki na kupelekea kufunga barabara kuu ya mjini, hali iliyompelekea Lowassa kupanda juu ya paa la  jengo la ofisi ya CCM Mkoa ili aweze kuzungumza nao.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 

Wednesday, June 17, 2015

PINDA APATA WADHAMINI NJOMBE




Mgombea wa Urais kupitia chama cha mapinduzi na waziri Mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda amewataka wananchama wa chama  cha mapinduzi Mkoa wa Njombe kuendelea kujitokeza kwa wingi na kuendelea kuwadhamini wagombea mbalimbali  waliochukua fomu na watakaochukua fomu  za kugombea nafasi ya  Urais bila kubagua Mgombea yoyote.
Waziri Mkuu ameyasema hayo leo kwenye ukumbi wa chama cha mapinduzi Mkoa wa Njombe ambapo mamia ya wananchama wa chama hicho  walijitokeza kumdhamini ili aweze kugombea Urais kupitia chama cha Mapinduzi
Alisema kuwa waliojitokeza kuchukua fomu kupitia chama cha mapinduzi ni wengi lakini atakayepitishwa kupitia chama hicho ni mgombea mmoja ambaye atawakilisha chama cha Mapinduzi kwenye uchaguzi unatakofanyika mwezi wa kumi na mgombea huyo ndie atanadiwa na chama hicho akishindanishwa na vyama vingine  kwenye uchaguzi Mkuu.
Wanachama waliojitokeza kumdhamini Mgombea huyo wamesema kuwa wanaimani kubwa na mgombea huyo na kuamini kuwa chama kitampitisha kuwakilisha chama hicho kwenye kugombea Urais.
Kwa Mkoa wa Njombe tayari wagombea January Makamba,Bernard Membe,Stive Wassira,Samweli Sitta,Makongoro Nyerere ,Monica Mbega ,Amosi Siyatemi na Prof.Mark Mwandosya.










Popular Posts