Tuesday, June 24, 2014

WATOTO WALIA NA WANAWAKE KWA KUWATUPA.


Kichanga kilichotupwa Iringa Sokoni.
ito umetolewa kwa kina mama na wadada waishio mkoani Iringa wenye tabia ya kupenda kutupa watoto pindi wanapojifungua kuacha kabisa kufanya kitendo hicho kwani wanapoteza Taifa la kesho.
Hayo yalisemwa na Kamanda wa polisi mkoani hapa ACP Ramadhani Mungi alipokuwa akizungumza na mtandao huu wa www.matukiodaima.com ofisini kwake kuhusiana na taarifa za kutupwa kwa mtoto kachanga maeneo ya karibu na ofisi ya Mkuu wa Wilaya.
“leo saa mbili asubuhi tulipokea taarifa ya kuwa kuna katoto kametupwa kwenye jalala lililopo karibu na ofisi ya Mkuu wa Wilaya, mtoto huyo ni wa jinsia ya kiume na hata kitovu chake bado hakijakatwa uchunguzi unaonyesha inawezekana kuna mtu alitoa mimba na akaenda kuitupa pale hivyo bado tunaendelea na uchunguzi na endapo tukimpata mtu huyu aliyefanya kitendo hicho cha kikatili basi hatua kali za kisheria zitachukuliwa, watu wanafanya kitendo hichi hawajui kuwa hawa wanaowatupa ndo Taifa la kesho huwezi jua huyo uliyemtupa angekuja kuwa nani mbeleni,” alisema Kamanda.
Tukio lingine, Jeshi la polisi mkoani Iringa linawashikilia watu wanne kwa kosa la kumchoma moto mwanafunzi wa Chuo cha Ruco aliyetambulika kwa jina la Daniel Lema (25) mkazi wa Kihesa mkoani hapa.
Kamanda alithibitisha kutokea kwa tukio hilo lililotokea mnamo tarehe 20 June majira ya saa 9 usiku huko maeneo ya Kihesa.
“majira ya saa 9 usiku polisi walipigiwa simu na wasamalia wema kutoka kihesa kuwa kuna mtu amefungwa kamba mikononi na anatembea huku anawaka moto mwilini polisi wakaenda eneo la tukio na kumkuta mtu huyo ameanguka chini huku bado anawaka moto basi polisi wakamfungua na kumpeleka hospitali kwani alikuwa bado anathema” alisema kamanda Mungi.
Kamanda alisema taarifa zinaonyesha kuwa mwanafunzi huyo ambaye yuko mwaka wan ne katika kitivo cha sheria alikuwa katika bar ya Inbox iliyopo kihesa akiangalia mpira, wakati akirudi kwake maeneo ya Transfoma alipitia kwenye grory grocery iliyopo pembezoni mwa grory lodge na kukuta imefungwa ambapo mlinzi alipomuona alimuita lakini mwanafunzi huyo alikimbia baada ya kumuona mlinzi akiwa na kirungu.
“mwanafunzi Yule alikimbia na mlinzi alimkimbiza na kumkamata ambapo alimpeleka kwa meneja wa hiyo lodge hata hivyo meneja huyo aliwapigia walinzi wengine kutoka katika kampuni ya Juka Security ili waje kumchukua kijana huyo wampeleke kituo cha polisi walinzi walifika wakiwa watatu na kumchukua mtu huyo ambapo walipofika mbele wakamfunga mikono yake na kamba na kisha kummwagia mafuta na kumchoma moto kisha wakakimbia.” Alisema.
Hata hivyo watuhumiwa hao walitaka kutoroka mkoani hapa mara baada ya kutenda kitendo hicho ambapo walikamatwa kabla hawajafanikiwa kutoroka, watuhumiwa hao ni Musa Nganga (28), Costa Mganyuko (38), Steven Kalolo (24) pamoja na Samson Peter (24) wote wakazi wa Kihesa, pia kwa upande wa mgonjwa hali yake sio nzuri bado.
NA DIANA BISANGAO WA MATUKIO DAIMA.COM, IRINGA  NA CHRISSMPUZU.BLONGSPORT.COM -NJOMBE

Monday, June 23, 2014

AJALI MBAYA MAENEO YA MAKONGO WATU ZAIDI 10 INASADIKIKA WAMEPOTEZA MAISHA PAPO HAPO :PICHA ZINATISHA

IMG_9044
 Mpaka sasa idadi kamili ya vifo vilivyotokana na ajali hii haijatangazwa ingawa baada ya ajali vifo viliyotajwa ni vya watu 6 ambapo ajali hii imehusisha magari mawili aina ya Coaster yanayosafririsha abiria kati ya Mwenge, Tegeta na Mbezi jiijini Dar.
Magari hayo yamegongana na kujeruhi ikiwa pamoja na kuua ajali hii imetokea mchana eneo la Makongo,baadhi ya mashuhuda wa ajali hii wamesema kuwa imesababishwa na uzembe uliofanywa na dereva wa daladala iliyokuwa ikitoka Tegeta kwa kupita upande usio wake.

IMG_9046 







IMG_9045

IMG_9042

UZEMBE…uzembe…uzembe ndiyo kauli ambayo ilitolewa na wananchi walioshuhudia ajali mbaya iliyohusisha magari mawili ya abiria (daladala) aina ya Toyota-Coaster maeneo ya Lugalo jijini Dar na kusababisha vifo vya watu sita na wengine 16 kujeruhiwa vibaya.


Uhalisia wa ajali iliyotokea Jumamosi (Juni 21, 2014) na kusababisha vifo vya watu sita na wengine 16 kujeruhiwa vibaya maeneo ya Lugalo. Ajali hiyo ilitokea juzi Jumamosi (Juni 21, 2014) ambapo kwa mujibu wa mashuhuda, chanzo kimetajwa kuwa ni uzembe wa dereva wa daladala iliyokuwa ikitokea Tegeta kwenda Mwenge ambayo ilichepuka na kuingia katika ‘saiti’ ya wanaokwenda Tegeta, ikaigonga ubavuni daladala nyingine iliyokuwa ikielekea  

 
Baadhi ya miili ya watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo.
“Dereva wa Coaster lililotokea Tegeta alikuwa spidi kuelekea Mwenge, alipoona kuna foleni katika upande wake, akachepuka ghafla kwenye maungio ya barabara na kulivaa ubavuni Coaster lililokuwa likielekea Tegeta,” alisema shuhuda huyo.
 
 

 












 





















TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Mjadala Bunge Maalum la Katiba halininyimi usingizi – Rais Kikwete
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa hana wasiwasi na hali ya mjadala mkali uliotawala Bunge Maalum la Katiba kwa sababu ni muhimu kwa mjadala kuhusu Katiba Mpya ukawa wa kina ili kuweza kupata Katiba bora kwa Watanzania.
Aidha, Rais Kikwete amesema kuwa Katiba ya Tanzania haitapatikana kwa mikutano ya kisiasa nje ya Bunge Maalum la Katiba bali ndani ya Bunge hilo ambako ni dhahiri kuwa mjadala utatawaliwa na nguvu ya hoja na busara.
Rais Kikwete ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama ametoa ufafanuzi huo mchana wa leo, Ijumaa, Juni 20, 2014, wakati alipotoa Mhadhara (Lecture) kuhusu Usalama wa Taifa (The Security of the Nation) kwenye Chuo cha Taifa cha Ulinzi – National Defence College – kilichoko Kunduchi, Dar Es salaam.
Wakati wa kipindi cha maswali na majibu, ofisa mmoja wa Jeshi la Kenya alimwuuliza Rais Kikwete kama alikuwa na wasiwasi kuhusu mjadala unaoendelea nchini kuhusu Katiba Mpya unaweza kuvuruga usalama wa Tanzania.
Rais Kikwete amemjibu: “Sina wasiwasi hata kidogo kwa sababu hatukutarajia kuwa mjadala wa Bunge Maalum la Katiba kuhusu jambo hili kubwa ungekuwa rahisi. Yalipojitokeza maoni ya Tanzania kupata Katiba Mpya, tuliunda Tume na tume hiyo ikatoa ripoti yake ambayo ndiyo inajadiliwa katika Bunge Maalum. Hatukutarajia kuwa mjadala kuhusu ripoti ungekuwa rahisi kwa wajumbe kutoa majibu ya ndiyo ama hapana.”
Ameongeza Rais Kikwete: “Kinachoendelea ni jambo muhimu na la lazima…najua wakati mwingine majadiliano yalikuwa makali mno lakini hili ni jambo zuri. Aina ya mfumo na muundo wa Serikali lilizusha mjadala mkali lakini hayo ni matokeo ya hali halisi ya masuala yanayojadiliwa.”
“Ni imani yangu kuwa tutafikia mwisho. Mwisho upi, hilo ni suala la Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kuamua. Muhimu ni kwamba Katiba Mpya inaweza kupatikana kutoka Bungeni tu siyo kupitia mikutano ya hadhara nje ya Bunge. Huko hakuna Katiba huko kuna mikutano ya hadhara na siasa tu. Katiba itapatikana kwa mijadala na kwa nguvu ya hoja ndani ya Bunge letu.”
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
IKULU
DAR ES SALAAM
20 Juni, 2014

Monday, June 16, 2014

NAPE ATINGISHA JIMBONI MNYIKA, LEO

Na Bashir Nkoromo, Dar es Salaam

KATIBU wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye,  leo ametoboa siri kwamba, viongozi wa ngazi ya juu wa Chadema wamelazimika kukumbatia kinachoitwa Umoja wa Katiba ya wananchi (UKAWA), ili kujaribu kupoza migogoro iliyopo ndani ya chama hicho ambayo inakiua.

Amesema, siyo kweli kwamba Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Woilbrod Silaa na Mwenyekiti wa Chama hicho Freeman Mbowe wanahangaika na muungano huo unaoitwa wa kutafuta Katiba ya Wananchi (UKAWA) kwa lengo la kusaidia wananchi bali ni kujaribu kupoza makali, baada ya kuona kwamba chama chao kimo katika mgogoro mkubwa wa ndani ambao si mda mrefu utaua.

"Chadema wapo katika mgogoro mkubwa kutokana na baadhi ya viongozi wake hasa wa ngazi za juu kukiendesha chama katika misingi ya ubaguzi.. na ndiyo sababu leo au hata kesho, Mbowe hawezi kuitisha kikao cha Baraza Kuu la chama hicho, na akijaribu kufanya hivyo anatimuliwa", alisema Nape.

Nape pia hakumuweka kiporo Mbunge wa jimbo la Ubungo, John Mwinyika, badala yake alimpasha kwenye mkutano huo kwamba, baada ya wananchi wa jimbo hilo kudanganyika na kumpa ubunge, sasa akae mkao wa kuondoka baada ya uchaguzi mkuu utakaofanyika 2014.

"Mnyika na Chadema yake tunawambia pango lao hapa jimbo la Ubungo  linamalizika rasmi mwaka 2014 na hatuma mpango wa kumuongezea, kilichobaki sasa ajiandae tu kuondoka taratibu", alisema Nape.

Alisema, Mnyika kama walivyo wabunge katika maeneo ambako wananchi walijaribu kuwachagua wapinzani, anachofanya yeye na Chama chake cha Chadema ni kupambana na kujenga misingi ya chama chao kuendelea kuwa kuishi na kamwe hawashughulikii matatizo ya wananchi.

"Na hili niliwaambia miaka mingi iliyopita, nilisema hapa ubungo kwamba mkimchagua mpinzani kazi yake itakuwa kutafuta njia za kuimarisha chama chake, na kamwe hataweza kujihusisha na masuala ya maendeleo yenu", alidai Nape na kuongeza;-

"Mnyika kama kweli una lengo la kuwatumikia wananchi wa Ubungo, umefika wakati wa kuacha sasa na mambo ya kudai kila mara hoja binafsi bungeni, sasa udai na hoja za wananchi, maana ukiendelea kudai hoja binafsi zaa wananchi utadai lini?"

Alisema, ni kutokana na wapinzani akiwemo Mnyika na chama chake cha Chadema, kutokwa mapovu midomoni kila kona ya nchi wakihangaika na Katiba mpya, tena wanachozungumzia zaidi serikalikali tatu na kusingizia kwamba ndiyo mahitaji ya wananchi huku wakijua wazi kwamba wanachohitaji wananchi kama wa Ubungo ni maji, elimu na afya na siyo idadi ya serikali.
 
Nape alisema hivi sasa wananchi wameshastukia vyama vya upinzani kwamba vipo kwa maslahi ya wachache ni si ya wananchi kama vinavyovyojinadi.

Alisema, miongoni mwa dalili za wananchi kuvistukia vyama cya upinzani, ni hali ilivyojitokeza wakati wa ziara za Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alkizofanya akiambatana na Nape mwenyewe mikoani.

Nape alisema, katika ziara hizo hadi sasa wanachama  12, 430 walijiunga CCM huku karibu nusu yao wakiwa wametoka katika vyama vya upinzani vikiwemo Chadema na CUF.

Katika mkutano huo ulioandaliliwa na Jumuia ya Wazazi mkoa wa Dar es Salaam, Nape alipokea wanachama wapya 480, wengi wao wakiwa wamehamia CCM kutoka katika vyama vya Chadema na CUF kwa nyakati tofauti.












  Mwenyekiti wa CCM, mkoa wa Dar es Salaam, Ramadham Madabiba akimlaki Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape  Nnauye alipowasili katika Kata ya Kimara kwa ajili ya ziara ya siku moja kukagua uhai wa Chama katika kata hiyo, leo Juni 15, 2014.


 Vijana wa Chipukizi wa CCM, wakimvisha skafu Nape alipowasili katika kata hiyo kuanza ziara ya siku moja leo,Juni 15, 2014. Kushoto ni Katibu wa Jumuia ya Wazazi mkoa wa Dar es Salaam, Mohamed Cholage na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge


WAFANYAKAZI WA KAMPUNI YA TANWAT KIBENA NJOMBE WALIPWA MSHAHARA WAO BAADA YA KUGOMA KWA SIKU MBILI

 
MWENYEKITI WA CHAMA CHA WAFANYAKAZI TPAW  AKIZUNGUMZA NA WAFANYAKAZI NA KUWATAKA WAWE NA MSHIKAMANO KATIKA KUDAI HAKI ZAO BWANA  SAMWEL HASSAN
 
 
 
 
 MWENYEKITI WA CHAMA CHA WAFANYAKAZI WA KAMPUNI YA TANWAT TPAW BWANA SAMWEL HASSAN AKIONGEZA NA WAFANYAKAZI HAO KWA KUWASIHI KUHUDHURIA MIKUTANO AMBAYO CHAMA HICHO HUWA KINAITISHA ILI KUJADILI MASWALA MBALIMBALI IKIWEMO MISHAHARA KUCHELEWESHWA PAMOJA NA UWEPO WA VIFAA VYA KAZI  KAMA SALE ZA KAZI.

Friday, June 13, 2014

MSICHANA ALIYEPEWA MATESO MAKALI NA KUCHOMWA NA PASI ARUHUSIWA KUTOKA HOSPITALI



Msichana  Yusta Lucas wa miaka ishirini aliyefungiwa ndani kwa miaka mitatu huku  akipewa adhabu ya kung'atwa na kuchomwa na pasi ameruhusiwa kutoka hopitalini baada ya hali yake kuendelea vizuri huku jeshi la polisi likikamilisha uchunguzi na mtuhumiwa kufikishwa mahakamani tarehe 11 Juni mwaka huu.
ITV imefika katika hospitali ya Mwananyamala alikokuwa amelizwa Yusta Lucus na kukutana na ndugu zake akiwemo mama ake mzazi ambaye amefafanua kwa uchungu hali aliyomkuta nayo binti yake na hatua alizochukua mara baada ya kupokea taarifa za tukio hilo.
Kaka wa Yusta licha ya kutoa shukrani kwa msamaria aliyetoo habari za mdogo wake kwa jeshi la polisi ameelezea kuendelea kusikitishwa na kitendo hicho cha kinyama na kutoa wito kwa Watanzania kuwa na moyo wa kusaidia wale wote wanaopatwa na matatizo kama
Msichana  Yusta Lucas wa miaka ishirini aliyefungiwa ndani kwa miaka mitatu huku  akipewa adhabu ya kung'atwa na kuchomwa na pasi ameruhusiwa kutoka hopitalini baada ya hali yake kuendelea vizuri huku jeshi la polisi likikamilisha uchunguzi na mtuhumiwa kufikishwa mahakamani tarehe 11 Juni mwaka huu.
ITV imefika katika hospitali ya Mwananyamala alikokuwa amelizwa Yusta Lucus na kukutana na ndugu zake akiwemo mama ake mzazi ambaye amefafanua kwa uchungu hali aliyomkuta nayo binti yake na hatua alizochukua mara baada ya kupokea taarifa za tukio hilo.
Kaka wa Yusta licha ya kutoa shukrani kwa msamaria aliyetoo habari za mdogo wake kwa jeshi la polisi ameelezea kuendelea kusikitishwa na kitendo hicho cha kinyama na kutoa wito kwa Watanzania kuwa na moyo wa kusaidia wale wote wanaopatwa na matatizo kama hayo.
Kamanda wa polisi mkoa wa Kipolisi Kinondoni Camillius Wambura amesema tayari uchunguzi umeshakamilika ikiwemo kumpima akili mtuhumiwa na tayari shauri hilo liko kwa mwanasheria mkuu wa serikjali na mtuhumiwa atafikishwa mahakamani tare 11 Juni mwaka huu.
 
 CREDITS:ITV
 
 
 
 
 
 
 

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA, MHESHIMIWASAADA MKUYA SALUM (MB) AKIWASILISHABUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI...

Hotuba Mawaziri fedha

 aziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum (Mb) akiwasilisha Bungeni hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara yake kwa mwaka 2014/15 leo mjini Dodoma. Waliokaa viti vya nyuma ni Manaibu Waziri Mwigulu Nchemba (kushoto) na Adam Malima (kulia).(Picha na Wizara ya Fedha).


Hotuba 1
Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum (Mb) akiwasilisha Bungeni hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara yake kwa mwaka 2014/15 leo mjini Dodoma.



ZIARA YA MWENYEVITI NA MAKATIBU KATA ZOTE 25 ZAIDI YA 91 MJINI DODOMA LEO KWA MWALIKO WA MBUNGE FILIKUNJOMBE NI ZIARA YA SIKU NNE DODOMA NA DAR ,MANGULA APONGEZA





 Baadhi ya makatibu  kati wa kata 25  za  wilaya ya  Ludewa  wakiwa katika makao makuu  wa CCM Dodoma  leo kwa  ziara ya  mbunge  Deo Filikunjombe kwa ajili ya kujifunza jumla ya  makatibu kata ya wenyeviti 92 wapo ziarani Dodoma na Dar kwa lengo ya kujifunza na  semina



 
 Baadhi ya  makatibu  wenezi  wa CCM kata 25  za jimbo la Ludewa

 

 Baadhi ya  wenyeviti wa kata 25  za jimbo la Ludewa  wakiwa makao makuu wa CCM Dodoma walipokutana na makamu mwenyekiti wa CCM bara Philip Mangula  leo





 

 Makamu  mwenyekiti bara Philip Mangula akiwa na mbunge  Deo Filikunjombe leo wakitoka makao makuu  ya  CCM Dodoma baada ya  kumaliza  ziara yao makao makuu ya CCM leo


















LOWASSA AKUTANA NA UJUMBE WA MBUNGE FILIKUNJOMBE DODOMA LEO ,ASEMA NI KWELI FILIKUNJOMBE JEMBE




 Waziri mkuu mstaafu Edward Lowasa kushoto akisalimiana na viongozi wa zaidi 91 wa jimbo la Ludewa mkoani Njombe ambao  wamefanya  ziara  Bungeni Dodoma leo ,jumla ya  wenyeviti 25 ,matatibu kata 25 makatibu  wenyezi 25 na viongozi  wengine wamefanya  ziara  bungeni  leo na makao makuu ya  chama kwa ufadhili  wa mbunge Filikunjombe  kesho  ni  ziara ya Dar katika mafunzo,katikati anayeshuhudia ni mbunge Filikunjombe


Wednesday, June 4, 2014

Mtoto aliyekuwa ndani ya boksi amezikwa kwa heshima zote.....Mazishi yameongozwa na mkuu wa mkoa wa Morogoro, Bofya hapa kuona picha za tukio hilo






 


MAZISHI YA BABAKE MKWE WA LUKUVI AYAFANYIKA LEO IRINGA





 Waziri  wa nchi ofisi ya  waziri mkuu sera na uratibu wa bunge Wiliam Lukuvi kushoto akiwa ameshika chombo  cha maji ya ibada ya mazishi akimsaidia paroko wa kanisa la RC kihesa  leo  wakati wa ibada ya mazishi ya  babake mkwe wa Lukuvi 





katibu  wa CCM mkoa  wa Iringa Hassan Mtenga akitoa heshima zake katika jeneza la mwili wa babake mkwe wa Lukuvi anayefuata nyuma ni mwanahabari Denis Mlowe





Wadau  mbali  mbali  wakiaga mwili wa babake mkwe  wa Lukuvi leo




wananchi mjini Iringa  wakitoa  heshima  zao











MAJANGA DEREVA NA UTINGO WAJIIBIA MALI WALIZOKUWA WAKISAFIRISHA KWENDA KONGO ZIKIWA NA THAMANI YA TSH MILIONI 100 ,WACHOMA LORI LILILOKUWA NA MZIGO HUO


 Kamanda  wa polisi  mkoa  wa Iringa Ramadhan Mungi kushoto akisalimiana na mwakilishi wa kampuni ya Dandu ambao lori lao limeteketezwa kwa moto .




Hii ndio  mitumba  iliyohifadhiwa mali ya wizi




Mitumba  hiyo ikionekana kwa nje baada ya kujaa ndani ya nyumba hiyo kupita kiasi



Safari ya kwenda  kubaini mali ya wizi iliyofanywa na kamanda wa polisi Iringa




RPC Iringa Ramadhan Mungi akiangalia  mitumba  iliyohifadhiwa porini baada ya  kuporwa 










kamanda wa  polisi Iringa Ramadhan Mungi akimwonyesha mmiliki wa nyumba iliyohifadhi  mali  hizo za wizi kulia na dereva wa gari hilo mbele lenye namba  T 185 CJM ambalo  ndilo lilikuwa likisomba mali  hizo za wizi kutoka katika  lori lililochomwa moto 





Watuhumiwa wa  wizi wa mali  zilizokuwa  zikisafirishwa na lori la kampuni ya Dandu





Kamanda wa polisi mkoa wa Iringa Ramadhan Mungi akionyesha  lori hilo mali ya kampuni ya Dandu ambalo limechomwa moto na dereva na utingo wake baada ya  kufaulisha mali zote kwa lengo la kuiba





JESHI la  polisi  mkoa  wa Iringa kupitia dhana ya polisi  jamii na ulinzi shirikishi  limefanikiwa  kukamata  mali za wizi ambazo zilizokuwa  zikisafirishwa kwenda nchi ya DRC Kongo zikiwa na thamani ya  Tsh milioni 100 pamoja na lori  lenye thamani  ya Tsh milioni 100 ambalo liliteketezwa kwa  moto kabla ya dereva na utingo wa  lori hilo  kulichoma moto kama njia ya kupoteza ushahidi.

Imedaiwa  kuwa  watu  zaidi ya 6  wanashikiliwa na  jeshi  hilo la polisi akiwemo  dereva  na utingo  wake ambao wanadaiwa  kuhusika na tukio  la wizi  huo.

Kamanda  wa  polisi mkoa  wa  Iringa Ramadhan Mungi  alisema  kuwa  tukio hilo  lilitokea juzi May 31 ambapo  askari  wa  doria  wilaya ya Mufindi  wakiwa katika shughuli   hiyo ya doria  walifanikiwa  kuliona  lori hilo  likiwa  limeegeshwa kando ya  barabara ya Iringa –Mbeya  eneo la Kinegembasi wilaya ya Mufindi  huku likiwa  limeteketea kwa moto katika kibini yake.

Alisema kuwa  watu hao waliteketeza lori lenye namba za usajili  T527 DPQ likiwa na tela lenye namba  T 974  EFE  aina ya  scania mali ya kampuni ya Dandu ambalo  walilikuta  likiungua   huku silizi  zake zikiwa  zimefunguliwa na  baada  ya uchungu wa awali  walibaini  kuwa lori hilo  lilikuwa limebeba mitumba na viatu  na baada ya msako  ndipo  walipofanikiwa  kukuta mitumba  hiyo  ikiwa imefichwa katika  nyumba moja kuukuu mali ya mama  Gray Mpinga  mwenyeji wa Maguhani Mufindi .

Alisema  kuwa mali  hizo ambazo ni mabelu ya mitumba na viatu  yalitoka Bandarini kwenda DRC  na kuwa dereva wa  lori hilo ni Enedia Christian (26) mkazi wa Mbeya  na utingo wake  Deus  Gendo (20) mkazi wa Mbeya .
Kamanda  Mungi  alisema kuwa utingo na dereva wa  lori hilo baada ya kufika kijiji  hicho cha Maguhani  walivunja kontena na  kushusha mali zote na kuzihifadhi katika  nyumba   hiyo kabla ya  kutafuta mteja na kisha  lori  kulichoma moto .

Alisema kuwa  baada ya  kufanya  wizi huo  walitoweka na simu zao kuzimwa na kutokana na jitihada za  jeshi la  polisi  kupitia mtandao wa kimawasiliano wa kuthibiti na wizi  wa mitandaoni  walifanikiwa  kuwanasa  watuhumiwa hao wakiwa kijiji cha Nyololo

Mbali ya kuwakamata  dereva na  tingo  pia  polisi  wamekamata  watu  mbali mbali  wahusika  wa mtandao huo na kuendelea  kumsaka Masko Buhewa mkazi wa Nyololo kwa  kuhusika na umilikiwa wa mtandao huo 
USIKOSE HABARI  HII  INAENDELEA ZAIDI













Popular Posts