Monday, January 12, 2015

HALMASHURI ZA MKOA WA NJOMBE ZATAKIWA KUTENGA MAENEO YA KWA AJILI YA SKAUTI.



HALMASHURI ZA MKOA WA NJOMBE ZATAKIWA KUTENGA MAENEO YA KWA AJILI YA SKAUTI.
Na,Christopher Philemon,Ofisa Habari Mkoa wa Njombe.

Halmashauri za Mkoa wa Njombe zimeagizwa kutenga maeneo ya kupanda miti kwa ajili kusaidia vikundi vya Skauti vilivyopo katika Shule za Msingi na Sekondari zilizopo katika Halmashuri zao.Pia wakuu wa Wilaya za katika Mkoa huo wamegizwa kuwa walezi wa Skauti katika wilaya zao.
Maagizo hayo yametolewa na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dr.Rehema Nchimbi leo tarehe 12 Januari 2015 aliyasema hayo kwenye sherehe ya kusimikwa kuwa mlezi wa Skauti Mkoa wa Njombe .
Katika Sherehe hizo zilizofanyika Ikulu ndogo ya Njombe ,Dr.Rehema Nchimbi aliweza kuuwapisha Makamishna watano wa wilaya za Makete,Ludewa,Njombe na Wanging’ombe.
Mkuu huyo wa Mkoa amewataka Skauti katika Mkoa wa Njombe kuwa Mfano wa kuigwa katika masomo,nidhamu na kufanya kazi kwa umoja  na upendo katika maisha yao ya kila siku na kuwataka vijana wengine na wazee kujiunga na Skauti kwani Skauti sio Jeshi bali ni vikundi vilioundwa kwa utaratibu maalum kwa ajili ya kufundisha Elimu,Upendo,nidhamu na mazoezi ya kukabiliana na maisha ya kila siku ya Mwanadamu.
Sarah Dumba Mkuu wa wilaya ya Njombe alisema kuwa Skauti katika Mkoa Njombe  wamekuwa Msaada mkubwa katika matukio mbalimbali kama vile maafa,sherehe na matukio mengine wamekuwa wametoa msaada mkubwa katika matukio hayo.
Kamishna wa Skauti Mkoa wa Njombe Tutsiwene K.Mahenge amesema kuwa kwa mkoa wa Njombe kunazaidi ya Skauti elfu tatu( 3000) ambao waanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari na kusema kuwa skauti hao huwa wanudhuria vipindi madarasani kama kawaida na skauti hao wanafanya mazoezi siku za Jumamosi.





Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dr.Rehema Nchimbi akiveshwa Skafu ya kuwa Mlezi wa Skauti Mkoa wa Njombe na mmoja wa Skauti Mkoa wa Njombe.





















No comments:

Post a Comment

Popular Posts