Thursday, January 22, 2015

NJOMBE KUPATA BILION TATU ZA KUBORESHA HUDUMA YA MAJI NJOMBE MJINI




Mkoa wa Njombe kupata zaidi ya bilioni tatu   kwa ajili ya Miradi ya kuboresha huduma ya maji Mjini Njombe,mradi huyo ni Nyenga na Mradi wa Ujenzi wa Mtandao wa Maji maeneo ya maji pamoja na eneo la Ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe,hayo yamesemwa na naibu waziri wa Moses Makala Kwenye ziara yake  ya siku mbili  iliyoanza jana ya kutembelea Miradi na vyanzo vya maji katika Mkoa wa Njombe.
Naibu waziri alisema kuwa mpaka sasa Mkoa wa Njombe umepokea billion mbili ( 2,177,138,890) kwa ajili ya  kusambaza maji maeneo ya Airport,Kambarage,Igeke,Mji mwema,Nazareti,Magereza na Nzengelendete.
Alisema kuwa wakandarasi tayari wanaendelea na kazi ya kujenga Manteki  matatu yenye lita135,000 katika maeneo la Mji mwema na Airport huduma ya maji inapatika kwa kutumia chanzo cha Nyenga che uwezo kwa kusambaza  maji eneo la Njombe Mjini.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira Njombe ( Njuwasa ) bwana Daudi Majani amemweleza naibu waziri kuwa miradi wa Nyenga  utakamilika ifikapo mwezi wa tatu mwaka 2015 na kufanya Mji wa Njombe  kuongezea huduma ya maji kutoka asilimia 43% hadi kufikia asilimia 79%.
Aliandelea kusema kuwa kwa ongezeko hilo la huduma ya maji kwa asilimia 79% itafanya malamka  kuongeza idadi ya wateja wake kutoka 4,450 hadi kufikia 5,450  na wateja wa kufungiwa dira za maji kuongezeka kutoka asilimia 67% ya sasa na kufika kwa asilimia 90% ya wateja wote.
Naibu waziri amemaliza ziara yake  ya siku mbili mkoani Njombe kwa kukutana na wadau wa maji katika mkoa huo kwa kuwataka watunze vyanzo vya maji ili mkoa huo uwendele kuwa na vyanzo vingi vya maji ili kuondoa tatizo la maji katika makoa wa Njombe.




Naibu waziri wa Maji Moses Makala wapili kutoka kulia akiapata maelezo ya matumizi ya kuunganisha bomba kwa kutumia plastic welding kutoka kwa mhandisi wa mamlaka ya maji mkoa wa Njombe Abiud Njangale,jana kwenye eneo la Air port ambapo maradi wa usambaji wa maji Mkoa wa Njombe unaendelea.( Picha Christopher Philemon)




 PICHA ZA ZIARA YA NAIBU WAZIRI WA MAJI MKOANI NJOMBE










No comments:

Post a Comment

Popular Posts